Uncategorized

WAZIRI NDALICHAKO ATETA NA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA DODOMA

Written by mzalendoeditor

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia (Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. ProfJoyce Ndalichako akizungumza katika kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria wakati wa kujadili na kupitisha taarifa Utekelezaji wa Bajeti ya mwaka wa fedha 2021/22 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2022/23 katika Ofisi za Bunge Machi 24, 2022 Jijini Dodoma.

Sehemu ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria wakifuatilia kikao hicho.

Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Mhe. Emmanuel Mwakasaka (Mb)akiongoza kikao cha kamati hiyo cha Kujadili na kupitisha Utekelezaji wa Bajeti ya mwaka wa fedha 2021/22 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2022/23 ya Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu pamoja na Taasisi zilizopo chini ya Ofisi hiyo.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Khadija Shabani akichangia hoja wakati wa kikao hicho.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Mwasi Kamani akichangia hoja katika kikao hicho.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia (Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. ProfJoyce Ndalichako akifuatilia hoja mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa wajumbe wa kamati hiyo wakati wa Kujadili na kupitisha Utekelezaji wa Bajeti ya mwaka wa fedha 2021/22 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2022/23 ya Ofisi. Kushoto ni Naibu Waziri kutoka katika ofisi hiyo, Mhe. Patrobas Katambi.

Baadhi ya Wakuu wa Idara kutoka Ofisi ya Waziri Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu wakifuatilia kikao cha kamati hiyo cha Kujadili na kupitisha Utekelezaji wa Bajeti ya mwaka wa fedha 2021/22 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2022/23 ya Ofisi hiyo.

                                

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

KAZI, VIJANA, AJIRA NA WATU WENYE ULEMAVU

About the author

mzalendoeditor