Featured Kitaifa

BARAZA LA WAWAKILISHI ZANZIBAR WAFANYA ZIARA EWURA

Written by mzalendoeditor

 

 

Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati Zanzibar, imefanya ziara kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ili kupata uzoefu wa shughuli za udhibiti leo tar. 6 Mei 2024.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Yahaya Rashid Abdala, ameishukuru EWURA kwa kuwakaribisha vizuri na kueleza imani yake kuwa watajifunza masuala mengi muhimu kuhusu udhibiti.

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Andilile, alisema EWURA ipo tayari wakati wote kutoa mafunzo na taarifa za masuala ya udhibiti kwa wadau mbalimbali nchini.

“Napenda kuwakaribisha sana EWURA, tumefarijika kwa ujio wenu, tutawapa ushirikiano wa hali ya juu ili lengo la ziara hii lifikiwe” Alisema.

Mada zitakazowasilishwa katika mafunzo hayo ni pamoja na majukumu na wajibu wa EWURA, Udhibiti wa mafuta, udhibiti wa gesi asilia, udhibiti wa sekta ya umeme, udhibiti wa majisafi na usafi wa mazingira, sheria na kanuni pamoja na masuala ya bei.

Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt James Andilile ( aliyesimama) akiwakaribisha wajumbe wa Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar walioitembelea EWURA kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu masuala ya udhibiti.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe Yahya Rashid Abdala, akiwaongoza wajumbe wakati wa mafunzo ya masuala ya udhibiti katika Ofisi za EWURA makao makuu jijini Dodoma.

Watendaji wa EWURA wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Dkt James Andilile( kulia) wakati wa semina kuhusu udhibiti wa huduma za nishati na maji kwa Wajumbe wa Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar iliyofayika makao makuu ya EWURA.

Wajumbe wa Kamati ya Mawasiliano Ardhi na Nishati wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakiendelea na semina kuhusu masuala ya udhibiti katika ofisi za EWURA Makao Makuu jijini Dodoma..

About the author

mzalendoeditor