Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), akipokea tuzo maalumu ya kutambua mchango wake katika Sekta ya Fedha, kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam, Bw. Peter Nalitolela (kushoto), katika hafla ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) yenye kaulimbiu “Miaka 30 ya Kuchochea Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uwekezaji Endelevu”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Mwenyekiti wa Bodi ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Daniel Ole Sumayan (kushoto nyuma) na Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), CPA Nicodemus Mkama (katikati).

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza katika hafla ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) yenye kaulimbiu “Miaka 30 ya Kuchochea Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uwekezaji Endelevu”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam, ambapo alieleza namna Serikali ilivyojipanga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha huduma za kifedha, masoko ya mitaji na uwekezaji katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Bara la Afrika kwa ujumla.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam, Bw. Peter Nalitolela, akizungumza katika hafla ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) yenye kaulimbiu “Miaka 30 ya Kuchochea Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uwekezaji Endelevu”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya Washiriki wa hafla ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) yenye kaulimbiu “Miaka 30 ya Kuchochea Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uwekezaji Endelevu”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam, wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), wakati akihutubia katika hafla hiyo.

Meza kuu ikiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (katikati), wakifuatilia Makala maalumu ya kuelezea historia ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), wakati wa hafla ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya DSE yenye kaulimbiu “Miaka 30 ya Kuchochea Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uwekezaji Endelevu”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.

Meza kuu ikiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (katikati), wakiwa katika picha ya pamoja na Wahitimu wa Kozi ya Uwekezaji na Uuzaji wa Hatifungani na Hisa (SIT), iliyoendeshwa na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), wakati wa hafla ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya DSE yenye kaulimbiu “Miaka 30 ya Kuchochea Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uwekezaji Endelevu”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.

Meza kuu ikiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (katikati), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), wakati wa hafla ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya DSE yenye kaulimbiu “Miaka 30 ya Kuchochea Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uwekezaji Endelevu”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dar es Salaam)
Na Joseph Mahumi, WF, Dar es Salaam
Serikali imejipanga kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha huduma za kifedha, masoko ya mitaji na uwekezaji katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Bara la Afrika kwa ujumla, kwa kuwa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) lina nafasi muhimu katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Hayo yamesema na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), wakati akihutubia katika hafla ya Maadhimisho ya Miaka 30 ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) yenye kaulimbiu “Miaka 30 ya Kuchochea Ukuaji Jumuishi wa Uchumi na Uwekezaji Endelevu”, iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
Mhe. Balozi Omar alisema katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwa DSE, soko hilo limekua kutoka kuwa taasisi yenye shughuli chache za uwekezaji na kuwa moja ya nguzo muhimu za mfumo wa kifedha nchini kwa kuwezesha kampuni, Serikali na taasisi zake kupata mitaji ya muda mrefu kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo.
“DSE imechangia kuimarisha uwazi, utawala bora wa kampuni, nidhamu ya kifedha na kuongeza ushiriki wa wananchi katika umiliki wa uchumi kupitia uwekezaji kwenye hisa, hati fungani za Serikali na kampuni, sukuk pamoja na mifuko ya uwekezaji” alisema Mhe. Balozi Omar.
Aidha, alieleza kufurahishwa na ongezeko la matumizi ya teknolojia katika uwekezaji, hususan kupitia huduma ya Hisa Kiganjani, ambayo imeongeza ushiriki wa wananchi katika soko la mitaji na kuimarisha ujumuishaji wa kifedha.
Mhe. Balozi Omar aliongeza kuwa, Serikali imeendelea kunufaika na maendeleo ya soko la mitaji kupitia uhamasishaji wa rasilimali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akitolea mfano Hati Fungani ya Miundombinu ya Samia, Hati Fungani ya Stawi ya TCB Bank pamoja na Hati Fungani ya Kijani ya Tanga UWASA.
Aidha, Mhe. Balozi Omar alisema utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025-2030 unahitaji sekta imara ya fedha na masoko ya mitaji yenye uwezo wa kukusanya akiba za muda mrefu na kuzielekeza katika uwekezaji wenye tija kwenye sekta za miundombinu, nishati, maji, viwanda, kilimo, madini, uchumi wa buluu, makazi, afya, elimu na uchumi wa kidijitali.
“Nawataka Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) pamoja na wadau wa sekta hii kuendelea kuimarisha mazingira ya maendeleo ya soko la mitaji kwa kuboresha mifumo ya udhibiti, kulinda maslahi ya wawekezaji, kurahisisha taratibu na kuhakikisha soko linaendelea kuwa la uwazi, ufanisi na kuaminika” alisema Mhe. Balozi Omar
Alitoa wito kwa taasisi za umma, mashirika ya umma na taasisi nyingine za kimkakati kutumia zaidi fursa za soko la mitaji kupata fedha za muda mrefu kwa ajili ya kufadhili miradi ya maendeleo badala ya kutegemea bajeti ya Serikali pekee, huku akihimiza Benki Kuu ya Tanzania (BoT), CMSA, DSE na taasisi nyingine husika kuendelea kuimarisha elimu ya fedha na uwekezaji kwa wananchi ili kujenga jamii yenye utamaduni wa kuweka akiba, kuwekeza na kushiriki kikamilifu katika umiliki wa uchumi wa nchi.
“Nasisitiza umuhimu wa DSE kuendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa, kuimarisha usalama wa mifumo ya kidijitali na kupanua huduma za uwekezaji kwa vijana, wanawake na wajasiriamali, huku akihimiza ushirikiano wa masoko ya mitaji barani Afrika ili kunufaika kikamilifu na fursa zinazotokana na Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA).
Kwa Upande Wao Mwenyekiti wa Bodi ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Bw. Daniel Ole Sumayan na Afisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam, Bw. Peter Nalitolela, walisema katika kipindi cha miaka 30 iliyopita, DSE imebadilika kutoka taasisi iliyokuwa ikitegemea ruzuku ya Serikali kwa asilimia 100 hadi kuwa kampuni inayojitegemea kifedha, inayopata faida na kuigawia Serikali gawio kila mwaka tangu ilipoorodheshwa katika soko la hisa mwaka 2016.
Walibainisha kuwa Mafanikio hayo yanaakisi ukuaji wa soko la mitaji nchini na mchango wake katika kuimarisha sekta ya fedha na uchumi wa Taifa huku katika kipindi hicho, kampuni 29, zikiwemo kampuni 22 za Tanzania na saba za kigeni, zimeorodhesha hisa zao katika DSE, huku matoleo 43 ya hati fungani za kampuni binafsi pamoja na hati fungani mbalimbali za Serikali yakiorodheshwa sokoni.
“Matumizi ya teknolojia yameongeza ushiriki wa wananchi katika uwekezaji, ambapo idadi ya akaunti za uwekezaji (CDS Accounts) imeongezeka kutoka akaunti 2,000 mwaka 1999 hadi kufikia zaidi ya akaunti 868,000 mwezi Juni 2026, hatua aliyoieleza kuwa ni ushahidi wa kuongezeka kwa uelewa na imani ya Watanzania katika masoko ya mitaji” alisema Bw. Sumayan.