Kaimu Kamishna, Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bw. Alex Haraba, akizungumza wakati akifungua kikao kazi kilichokutanisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kufanya mapitio ya kupitia upya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa lengo la kuioanisha na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya St. Gasper, jijini Dodoma.

Kamishna Msaidizi wa Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bi Emma Komba, akichangia hoja katika kikao kazi cha kufanya mapitio ya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa lengo la kuioanisha na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya St. Gasper, jijini Dodoma.

Meneja Msaidizi, Tenda na Mikataba kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Magnus Mlokota, akitoa maoni katika kikao kazi cha kupitia upya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa lengo la kuioanisha na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya St. Gasper, jijini Dodoma.

Mwakilishi kutoka Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Bw. Berry Yongolo, akitoa maoni katika kikao kazi cha kufanya mapitio ya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa lengo la kuioanisha na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya St. Gasper, jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Jumbo, Bw. Mathias Luoga, akitoa maoni katika kikao kazi cha kupitia upya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa lengo la kuioanisha na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya St. Gasper, jijini Dodoma.

Baadhi ya wadau wakifuatilia hoja zilizokuwa zikiwasilishwa katika kikao kazi cha kupitia upya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa lengo la kuioanisha na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya St. Gasper, jijini Dodoma.

Kaimu Kamishna, Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bw. Alex Haraba, akiwa katika picha ya pamoja na wadau baaada ya kuhitimisha katika kikao kazi cha kufanya mapitio ya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa lengo la kuioanisha na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya St. Gasper, jijini Dodoma. Kulia ni Kamishna Msaidizi wa Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bi Emma Komba na kushoto ni aliyekuwa Katibu wa Kikao kazi hicho ambaye ni Mwanasheria kutoka Idara ya Sheria, Wizara ya Fedha, Bw. Paul Kimweri.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dodoma.)
Na. Saidina Msangi, WF, Dodoma.
Wizara ya Fedha inaendelea na mchakato wa kupitia upya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa lengo la kuioanisha na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kupitia kikao kazi kilichowakutanisha wadau mbalimbali kutoka sekta ya umma na binafsi.
Mchakato huo umeanza kwa kikao kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper, Jijini Dodoma, ambapo wadau walipata fursa ya kutoa maoni na mapendekezo yatakayosaidia kuboresha Sheria hiyo.
Akifungua kikao hicho, Kaimu Kamishna wa Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bw. Alex J. Haraba, alisema mapitio hayo yanalenga kujenga mfumo wa kisasa unaojumuisha hatua zote za mnyororo wa ugavi, kuanzia upangaji wa mahitaji, ununuzi, upokeaji na ugomboaji, uhifadhi na utunzaji, usambazaji, hadi uondoshaji wa mali.
‘‘Mapitio ya sheria hii ni hatua ya kimkakati ya kuhakikisha kuwa masuala yote yanayohusu mnyororo mzima wa ugavi yanajumuishwa kikamilifu katika Sheria mpya, na kwamba mageuzi hayo yatakuwa chachu ya kuchochea maendeleo ya Taifa kwa kuzingatia nguzo na malengo ya Dira ya Maendeleo 2050, ikiwemo ukuaji wa uchumi, maendeleo ya viwanda, pamoja na maendeleo jumuishi na endelevu’’, alisema Bw. Haraba.
Aliongeza kuwa Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, imeipa Wizara ya Fedha jukumu la kisheria la kupitia na kuhuisha sera, sheria, kanuni, miongozo, pamoja na maelekezo mbalimbali yanayohusu ununuzi wa umma na ugavi nchini.
Bw. Haraba alifafanua kuwa maoni yote yatakayowasilishwa yatachambuliwa kwa kina ili kubaini maeneo ya kuboresha na kuweka misingi imara itakayosaidia Taifa kufikia malengo ya Dira ya Maendeleo 2050.
Aidha, Bw. Haraba aliwahimiza wadau kushiriki kikamilifu kutoa maoni na kukisisitiza kuwa ushiriki wao ndio utakaohakikisha Sheria mpya inakuwa bora, jumuishi na yenye tija kwa maendeleo ya Taifa.
Aliongeza kuwa Wizara ya Fedha itazingatia na kufanyia kazi mapendekezo yote yatakayowasilishwa katika hatua zinazofuata za mapitio hayo.
Kikao hicho, kilichoratibiwa na Wizara ya Fedha kupitia Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma, kiliwakutanisha pamoja wadau mbalimbali kutoka Sekta ya umma na binafsi.
Kwa upande wa sekta ya umma, taasisi zilizoshiriki ni pamoja na Tume ya Mipango, Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA), Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA), Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), Wakala wa Majengo (TBA), Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA), Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), pamoja na Bodi ya Usajili wa Wabunifu wa Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB).
Kwa upande wa sekta binafsi, walishiriki wazabuni mbalimbali wakiwemo Jali Motors Ltd, Firebrand Technologies, Primezone Ltd, Mr. Jumbo, Dynatech Solution Ltd, Vera International Travelling Agency, New Jari Fashion Ltd na Blueberry Travel, ambao walipata fursa ya kuwasilisha maoni yao kuhusu namna ya kuboresha mazingira ya biashara na ushiriki wao katika shughuli za ununuzi wa umma na ugavi.