marsbahis giriş

deneme bonusu veren siteler

Hacklink panel

Hacklink Panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Backlink paketleri

Hacklink Panel

Hacklink

Hacklink

Hacklink

Hacklink

Hacklink

Hacklink panel

Eros Maç Tv

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink satın al

Hacklink satın al

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Illuminati

Hacklink

Hacklink Panel

Hacklink

Hacklink Panel

Hacklink

Masal oku

Hacklink Panel

Hacklink Panel

meritking

Hacklink panel

Masal Oku

Hacklink

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink Panel

Hacklink

Hacklink

Hacklink

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink

Hacklink

Buy Hacklink

Hacklink

Hacklink

Hacklink satın al

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Hacklink panel

Masal Oku

Hacklink panel

หวยออนไลน์

Hacklink satın al

Hacklink Panel

unblocked games

unblocked games 76

meritking giriş twitter

new unblocked games

totalsportek

retro bowl

betpas, betpas giriş, betpas güncel

casibom

Brain Savior Review

holiganbet

https://guinguinbali.com/

boostaro review

casibom

holiganbet giriş

NervEase

mersin escort

sapanca escort

escort bayan

imajbet

vdcasino

güvenilir bahis siteleri

ganobet

bets10 giriş

ultrabet giriş

pusulabet giriş

grandpashabet

jojobet

dizipal

1xbet giriş

1xbet

tambet

bahiscasino

marsbahis

perabet giriş

imajbet

grandbahis

betpipo giriş

imajbet

betpipo

grandbahis giriş

jojobet

kulisbet giriş

pusulabet giriş

kulisbet, kulisbet giriş

ultrabet, ultrabet giriş

tlcasino, tlcasino giriş

alobet, alobet giriş

kingroyal

restbet

jojobet giriş

casibom

สล็อตออนไลน์ theprepperwebsitepodcast com

superbetin

trimology review

celtabet

meritking giriş

meritking

jojobet

holiganbet

holiganbet

holiganbet

holiganbet giriş

Nitric Boost

savoycasino giriş

starzbet

bahiscasino, bahiscaasino giriş

tipobet

jojobet

retro bowl

retro bowl unblocked 76

jojobet

bilgi kutusu

holiganbet

holiganbet giriş

alpha fuel pro

Alpha Fuel Pro

trimology review

Nitric Boost Ultra

tümbet giriş

tümbet

tümbet

tümbet giriş

starzbet

pokerklas

grandpashabet giriş

jojobet

jojobet güncel giriş

jojobet

jojobet giriş

jojobet

betturkey

betturkey giriş

pokerklas giriş

pokerklas giriş

pokerklas

betsmove

tümbet

tümbet giriş

tümbet giriş

tümbet

deneme bonusu veren siteler

casibom

jojobet güncel giriş

betsat

betsat giriş

xslot

xslot giriş

vaycasino

trendbet

bets10

Milanobet

jojobet

cratosroyalbet

deneme bonusu veren siteler

İkimisli

onwin

superbetin

bahibom

marsbahis

betsin

casino zonder cruks

vdcasino

vdcasino

vdcasino

bets10

padişahbet

holiganbet

perabet

perabet giriş

imajbet

imajbet giriş

perabet

imajbet

perabet

perabet giriş

Hacklink Panel

Hacklink Panel

Hacklink Panel

ankara escort

cratosroyalbet giriş

Hacklink Panel

สล็อตเว็บตรง

jojobet

Hacklink Panel

Hacklink Panel

Hacklink Panel

deneme bonusu veren siteler

Hacklink Panel

esbet

vdcasino

vaycasino giriş

perabet

perabet

perabet giriş

imajbet

imajbet giriş

imajbet

kralbet giriş

elitbahis

สล็อตเว็บตรง

zirvebet

superbetin

jojobet

jojobet

jojobet

trust score weak 3

jojobet

deneme bonusu veren siteler

deneme bonusu

imajbet

imajbet giriş

jojobet

casibom

casibom

jojobet güncel giriş

casibom

dinamobet giriş

netbahis

1xbet giriş

vipslot

bahis siteleri

interbahis

agb99

safirbet

Hacking forum

trend hack methods

avşa kiralık daire

betturkey giriş

betturkey

betturkey

betturkey giriş

deneme bonusu

1xbet

lefkoşa night club

deneme bonusu

sekabet giriş

hackhaber

grandpashabet

deneme bonusu veren siteler

eminevim

tipobet

tipobet giriş

galabet, galabet giriş

bahiscasino, bahiscasino giriş

roketbet, roketbet giriş

Uncategorized

MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII INAONDOA UTEGEMEZI UZEENI

Written by mzalendo

 

Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bi. Janeth Hiza, akitoa mada kuhusu elimu ya fedha kwenye mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa faida ya wazee na wastaafu, wakati wa mafunzo ya huduma za fedha kwa wasanii kutoka Shirika la TACCI mkoani Morogoro, watakao husika kutoa elimu ya fedha vijijini.

Mkurugenzi wa Shirika la Kijamii linalojishughulisha na utoaji wa Elimu ya Uraia TACCI, Bi. Aline Augustin na Mtaalamu wa Sanaa za Jukwaani, Bw. Harrison Kisaka, wakisikiliza mada ya uwekaji akiba, wakati wa mafunzo ya huduma za fedha kwa wasanii kutoka Shirika la TACCI mkoani Morogoro, ambao wanalengwa kutoa elimu ya fedha vijijini.

Afisa Msimamizi wa Fedha Mkuu kutoka Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bw. Salim Khalfan Kimaro,akielezea kuhusu umuhimu wa kuweka akiba akiba yenye malengo kwa Wasanii kutoka Shirika la Kijamii linalojishughulisha na utoaji wa Elimu ya Uraia (TACCI), mkoani Morogoro.

Msanii kutoka Shirika la Kijamii linalojishughulisha na utoaji Elimu ya Uraia, Bw. Rajabu Athuman Zegegia ambae ni mcheza ngoma, akiuliza jambo wakati wa mafunzo ya huduma za fedha kwa wasanii kutoka Shirika la Kijamii linalojishughulisha na utoaji Elimu ya Uraia – TACCI, mkoani Morogoro, ambao wanalengwa kutoa elimu ya fedha vijijini.

Msanii kutoka Shirika la Kijamii linalojishughulisha na utoaji wa Elimu ya Uraia, Bw. Iddy Athumani, ambae ni muingizaji, akieleza changamoto wanazoziona kwa watoa mikopo wasio sajiliwa wakati wa mafunzo ya huduma za fedha kwa wasanii kutoka Shirika la Kijamii linalojishughulisha na utoaji Elimu ya Uraia -TACCI, mkoani Morogoro, ambao wanalengwa kutoa elimu ya fedha vijijini.

Afisa Msimamizi wa Fedha Mkuu kutoka Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bw. Salim Khalfan Kimaro (wa saba kulia) na Mkurugenzi wa Shirika la Kijamii linalojishughulisha na utoaji wa Elimu ya Uraia TACCI, Bi. Aline Augustin (wa sita kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na maafisa kutoka Wizara ya Fedha na Wasanii kutoka TACCI, baada ya mafunzo ya elimu ya fedha mkoani Morogoro, yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kupeleka elimu hiyo maeneo ya vijijini.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Morogoro)

Na. Peter Haule, WF, Morogoro

Wananchi wanatakiwa kupata elimu ya fedha na kujiunga na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ili kuwasaidia wanapozeeka au kustaafu kazi ili kuondoa utegemezi.

Wito huo umetolewa mkoani Morogoro na Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bi. Janeth Hiza, wakati wa Mafunzo ya Elimu ya Fedha kwa Wasanii kutoka Shirika la Kijamii linalojishughulisha na utoaji wa Elimu ya Uraia (TACCI) wanaolengwa kupeleka elimu ya fedha vijijini.

Alisema kuwa Serikali imeweka Sera, Sheria, Kanuni na miongozo ambayo inamtaka kila mwajiri awe sekta ya umma au binafsi kuwaandalia wafanyakazi wake utaratibu wa kupata mafao baada ya kustaafu kwa ugonjwa, kufukuzwa kazi au kustaafu kwa kigezo cha umri.

“Kwa binadamu aliye kamilika anahitaji fedha na matumizi, kama ukiwa na fedha nyingi wakati wa ujana kuna wakati utafika nguvu zitaisha jambo litakalokufanya uhitaji Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ukusaidie ili uishi maisha yenye staha uzeeni, hapo ndipo linapokuja suala la umuhimu kujiunga kwenye mifuko ya Hifadhi ya Jamii”, alieleza Bi. Hiza.

Akitoa mada katika Mafunzo kwa Wasanii wa TACCI, Afisa Msimamizi wa Fedha Mkuu kutoka Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bw. Salim Khalfan Kimaro, alisema kuwa elimu ya fedha inamsaidia kila mtu kupanga maisha kwa ufasaha kwa kufahamu umuhimu wa usimamizi wa fedha binafsi, kutambua umuhimu wa kuweka akiba na eneo sahihi la kukopa

Vilevile alisema kuwa elimu ya fedha inasaidia mtu kuelewa umuhimu wa kulipa madeni anapokopa pamoja na kuzifahamu na kuzichangamkia fursa nyingine zinazopatikana katika sekta ya fedha zikiwemo uwekezaji katika mitaji ya dhamana.

“Katika ngazi ya mtu binafsi usipokuwa na elimu sahihi katika utekelezaji wa jambo lolote ni rahisi kushindwa kufikia malengo na kuwatupia lawama watu wengine ambao hawahusiki na kushindwa kwako”, alisema Bw. Kimaro.

Bw. Kimaro alisema program ya elimu kupitia Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha inayotolewa na Wizara ya fedha inasaidia kujua ni kundi lipi na idadi gani na wapi elimu inatakiwa kutolewa ili kutoa uelewa wa kutosha kwa wananchi, kuwawezesha kuingia katika kadhia ya hasara inayotokana na uelewa mdogo wa masuala ya fedha.

Alieleza kuwa Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha unalengo la kuhakikisha hadi kufikia mwaka 2025, asilimia 80 ya wananchi wawe na uelewa wa kutosha wa elimu ya fedha.

Alibainisha kuwa Walengwa wa program ya elimu ya fedha ni watumishi wa umma, wanafunzi, wakufunzi, wanawake, vijana, watu wenye mahitaji maalum, wajasiliamali wadogo na wa kati, asasi za kiraia, wahariri na waandishi wa vyombo vya habari, watoa huduma za fedha, Watoto na umma kwa ujumla.

“Maendeleo ya Sekta ya Fedha yatasaidia upatikanaji na ugawaji wa rasilimali fedha kwa ukuaji wa uchumi na kuondoa umasikini, fani pekee ambayo kila mtu anapaswa kuwa nayo ni elimu ya fedha kwa kuwa kila kazi inayofanywa ina sehemu ya kutafuta fedha,”, alisisitiza Bw. Kimaro

Kuhusu Sekta ndogo za fedha, Bw. Kimaro alisema zinajumuisha, Benki, Bima, Hifadhi ya Jamii, Masoko ya Mitaji na Dhamana na watoa huduma ndogo za Fedha (Micro Finance)

Kwa upande wake Mtaalamu wa masuala ya fedha wa Wizara ya Fedha, Bi. Grace Muiyanza alisema kuwa Watoa huduma za fedha wapo katika madaraja manne, Daraja la kwanza linahusika na Benki na daraja la pili ni wale ambao hawapokei amana (wakopeshaji binafsi na kampuni) ambapo madaraja hayo yanasimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT)

Alieleza kuwa Daraja la tatu ni wale wanapokea amana ambao wanasimamiwa na Tume ya Maendeleo ya Ushirika na daraja la nne ni vikundi vya kijamii vya huduma ndogo za fedha (CMG), ambavyo vinasimamiwa na TAMISEMI, mamlaka ambayo wamekasimishwa na Benki Kuu ya Tanzania-BoT

Bi. Muiyanza alieleza kuwa vikundi vya kijamii vya watoa huduma ndogo za fedha ambavyo vipo daraja la nne vinatakiwa kuhusisha wanakikundi kuanzia 10 hadi 50 wenye malengo ya aina moja.

Aliongeza kuwa baada ya uongozi wa kikundi kuridhia kusajili kikundi, wanatakiwa kuandaa taarifa za msingi kupitia portal na kuwasilisha Mamlaka za Serikali za mitaa, Halmashauri, Manispaa au Jiji kwa ajili ya mapitio ya awali na kama taarifa zao zitakuwa sahihi zitarudishwa kwenye kikundi zikiwa na cheti cha usajili wa kikundi.

Bi Muiyanza alisema kuwa Taarifa za msingi zinazotakiwa ni pamoja na muhtasari wa kikao cha uanzilishi, orodha ya wanakikundi walioonesha nia ikiwa ni pamoja na michango ya awali waliyoitoa, barua ya utambulisho ya kata au Kijiji, katiba ya kikundi iliyoridhiwa kuitumia na wanakikundi wote.

Alifafanua kuwa Katika zoezi la kuwezesha usajili wa kikundi, wanakikundi wenyewe wanaweza kuingia kwenye tovuti na kufanya usajili au wakamhusisha Afisa maendeleo ya jamii aliyepo kwenye Mamlaka ya Serikali ya Mtaa au wakamtumia mhamasishaji wa biashara za huduma ndogo za fedha.

Aidha Bi. Muiyanza alisema kuwa Mhamasishaji anatakiwa kuwa mtu mwenye weledi kwenye masuala ya fedha lakini awe amesajiliwa katika Mamlaka ya Serikali ya Mtaa na amepata elimu ya masuala ya fedha, usimamizi na uendeshaji wa vikundi.

About the author

mzalendo