Featured Michezo

PHIRI AIPELEKA SIMBA MAKUNDI CAF

Written by mzalendoeditor

Na.Alex Sonna_MZALENDO BLOG 

SIMBA wametinga hatua ya Makundi Ligi ya Mabingwa barani Afrika baada ya kuichapa bao 1_0  De Agosto ya Angola mchezo uliomalizika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Shujaa wa Simba ni  Moses Phiri aliyefunga bao  dakika ya 33 akimalizia pasi ya HusseinTshabalala .

Kwa ushindi huo Simba wameitoa De Agosto kwa Jumla ya mabao 4_1 baada ya mechi ya awali nchini Angola kumalizika kwa Simba kushinda mabao 3-1.

About the author

mzalendoeditor