Featured Kitaifa

RAIS SAMIA AZIAGIZA TAKUKURU NA ZAECA KUFUATILIA MIRADI YA MAENDELEO ILIYOBAINIKA NA DOSARI

Written by mzalendoeditor

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kiongozi wa mbio hizo Kitaifa Sahil Geraruma katika Maadhimisho ya Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika kwenye uwanja wa Kaitaba, Bukoba Mkoani Kagera 

……………………………..

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameziagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) kufuatilia miradi ya maendeleo iliyobainika kuwa na dosari. 

Rais Samia ametoa agizo hilo leo kwenye hafla ya Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2022 na kumbukumbu ya Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere iliyofanyika katika Uwanja wa Kaitaba. 

Aidha, Rais Samia amezitaka TAKUKURU na ZAECA kuwachukulia hatua wasimamizi wa miradi iliyobainika kuwa na ufujaji, wizi, matumizi mabaya ya fedha, pamoja na rushwa.

Rais Samia pia amesema vitendo vya rushwa vinajirudia kwa kuwa Viongozi katika maeneo mbalimbali hawafuatilii maendeleo ya miradi ya wananchi hadi Mwenge wa Uhuru unapopita na kubaini dosari hizo katika miradi hiyo. 

Vile vile, Rais Samia amewataka Viongozi na watendaji wahakikishe wanasimamia matumizi sahihi ya fedha zinazoelekezwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Rais Samia pia amekemea tabia ya baadhi ya viongozi wasiojali na kuhurumia wananchi kwa kuwapa miradi Wakandarasi wasio na uwezo na kusababisha miradi kutotekelezwa ipasavyo. 

Mbio za Mwenge wa Uhuru zilizinduliwa tarehe 02 Aprili, 2022 ambapo miradi ya maendeleo 1293 iliyogharimu shilingi bilioni 650.8 ilizinduliwa na kuwekwa mawe ya msingi katika maeneo mbalimbali hapa nchini.  

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kiongozi wa mbio hizo Kitaifa Sahil Geraruma katika Maadhimisho ya Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika kwenye uwanja wa Kaitaba, Bukoba Mkoani Kagera tarehe 14 Oktoba, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Kagera katika Maadhimisho ya Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo yamefanyika kwenye uwanja wa Kaitaba, Bukoba Mkoani Kagera tarehe 14 Oktoba, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wananchi wakati akiwasili kwenye uwanja wa Kaitaba, Bukoba Mkoani Kagera kwa ajili ya kushiriki Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika Mkoani humo tarehe 14 Oktoba, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akivalishwa Skafu na Vijana wa Skauti mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Kaitaba kwa ajili ya kushiriki Maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo Kitaifa yamefanyika Mkoani Kagera tarehe 14 Oktoba, 2022.
 
 
 
 
Vijana wa Halaiki wakitumbuiza kwa kuonesha kazi mbalimbali katika Kilele cha Maadhimisho ya Mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo yamefanyika kwenye uwanja wa Kaitaba, Bukoba Mkoani Kagera tarehe 14 Oktoba, 2022.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa vyeti kwa wakimbiza mwenge Kitaifa katika kilele cha mbio za Mwenge mkoani Kagera tarehe 14 Oktoba, 2022.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye uwanja wa Kaitaba, Bukoba Mkoani Kagera kwenye Maadhimisho ya Kilele cha Maadhimisho ya mbio za Mwenge wa Uhuru ambayo yamefanyika kwenye uwanja wa Kaitaba, Bukoba Mkoani Kagera tarehe 14 Oktoba, 2022.

About the author

mzalendoeditor