Featured Kitaifa

WADAU WA MALEZI NCHINI KUJIKITA KATIKA ELIMU MALEZI CHANYA KWA MTOTO

Written by mzalendoeditor

 Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mtoto kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Sebastian Kitiku akizungumza na wadau wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto  kwenye Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto wakati wa kikao kilichofanyika jijini Dodoma.

 Mkurugenzi wa Mtandao wa Malez,i Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto Mwajuma Rwebangira akielezea lengo la mradi wa Mtoto Kwanza kwa wadau wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto, kwenye  Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto katika kikao kilichofanyika jijini Dodoma.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika Bright Jamii Iniatitive Irene Fugala akichangia mada kwenye  kikao cha wadau wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto chenye lengo la kuwapitisha wadau wa Mradi wa Mtoto Kwanza kwenye Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto katika kikao kilichofanyika jijini Dodoma.

Meneja Programu kutoka Shirika KIHUMBE Jeremia Henry akichangia mada wakati  kikao cha wadau wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto chenye lengo la kuwapitisha wadau wa Mradi wa Mtoto Kwanza kwenye Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto wakati  wa kikao kilichofanyika jijini Dodoma.

Baadhi ya wadau wa Malezi na makuzi ya Awali ya Mtoto kutoka Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, Idara na Taasisi za Serikali wakishiriki kikao cha kuwapitisha kwenye Mradi wa Mtoto Kwanza katika  Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto katika kikao kilichofanyika jijini Dodoma.

Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WMJJWM

……………………………………………………….

Na WMJJWM-Dodoma

Wadau wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto kupitia mradi wa Mtoto Kwanza wamejipanga kujikita kutoa elimu ya Malezi kwa jamii ili isadie kuondokana na mmomonyoko wa maadili unaochangia kutokea kwa vitendo vya ukatili.

Hayo yamebainika jijini Dodoma wakati wa kikao kilicho wakutanisha wadau hao kwa lengo la kuwapitisha kwenye Mradi huo katika utekelezaji wa Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto.

Mkurugenzi wa Shirika la Bright Jamii Initiative Irene Fugara alisema Shirika lake limejikita  kuhakikisha linatoa  elimu ya Malezi kwa Mtoto ili kupambana na ukatili wa kijinsia  dhidi ya Watoto ili  iweze kusaidia kuondoka na tatizo hilo.

“Lazima tuijengee jamii uwezo wa kuwa na uelewa kwenye masuala ya Malezi ili iwasaidie katika kuhakikisha watoto wanalelewa kwenye mazingira mazuri na yatakayowawezesha kuwa wazalendo, jasiri na wenye kujiamini ” alisema Irene

Naye Meneja Programu kutoka Shirika la KIHUMBE Jeremia Henry amesema Shirika hilo linashirikiana na Serikali na wadau wa maendeleo hasa upande wa  miradi ya watoto na vijana katika masuala ya Afya, Malezi, Makuzi, na pamoja na Lishe ndani ya jamii. 

“Kupitia Programu hii Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto tumepata uelekeo utakaotusaidia kuona ni namna gani tutatoa elimu ya Malezi kwa  jamii ili tuwe na jamii yenye watu wenye Malezi bira” alisema Jeremia 

Akifungua kikao hicho Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mtoto kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Sebastian Kitiku alisema Serikali imeweka jitihada mbalimbali ili kuhakikisha jamii inapata elimu ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto kwa kuzindua  Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto inayolenga kusaidia kutoa elimu ya Malezi chanya ndani ya jamii.

Mkurugenzi huyo alisema pia uwepo wa Programu hiyo nchini utasaidia kujiamini kwa kujenga kizazi chenye  kung’amua changamoto mbalimbali katika jamii na kuzifanya fursa za kimaendeleo katika jamii husika.

“Programu hii imeandaliwa na kuzinduliwa kwa lengo la kuziba mapengo yaliyopo kwa sasa, kwakua na mipango na Programu zingine za Malezi kwa Mtoto, hivyo itasaidia kutatua changamoto ziliziokuwepo miongoni mwa jamii hasa kwenye  Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto ” alisema Kitiku.

Akizungumza kwenye kikao hicho, Mkurugenzi wa Mtandao wa Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto Mwajuma Rwebangira alisema lengo la kikao hicho  ni kuwapitisha wadau wa Mradi wa Mtoto Kwanza katika Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto ili waweze kutumia Programu hiyo katika kutoa elimu kwa jamii kuhusu Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto.

“Sisi wadau wa Mtoto Kwanza katika kutekeleza mradi huu tuhakikishe tunatumia Programu hii ili kuhakikisha tunajikita katika kutoa elimu ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto katika sehemu tunazotoka” alisema Mwajuma

About the author

mzalendoeditor