Uncategorized

VIVUTIO VYA UTALII VYA TANZANIA KUTANGAZWA KUPITIA SHIRIKA LA NDEGE LA EMIRATES KUTAZAMWA NA ABIRIA WAPATAO MILIONI 90.2

Written by mzalendoeditor

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akizungumza  na Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu la Emirates, Badr Abbas kuhusu kuitumia ndege hizo katika  kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania ambapo ndege hizo  husafirisha abiria milioni  90.2 kwa kila  mwaka, Mazungumzo hayo yamefanyika  leo katika makao makuu ya Shirika hilo lililopo katika Mji wa  Dubai,  Wa pili kulia ni  Meneja wa Masoko wa Afrika wa Shirika hilo Muhamed Riz pamoja na Balozi mdogo wa Tanzania Dubai, Idd Bakari
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Afrika wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu  la Emirates, Badr Abbas jinsi vivutio vya utalii vya Tanzania vitajulikana klupitia  ndege hizo kwani Emirates husafirisha abiria  wapatao  90.2 kwa kila  mwaka, Mazungumzo hayo yamefanyika  leo katika makao makuu ya Shirika hilo lililopo katika Mji wa  Dubai,  Wa pili kulia ni  Meneja wa Masoko wa Afrika wa Shirika hilo Muhamed Riz  akiwa na Balozi Mdogo wa Dubai,  Idd Bakari
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akimuonesha picha ya baadhi ya vivutio vya utalii vya Zanzibara  Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Afrika wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu  la Emirates, Badr Abbas mara baada ya kuona picha ukutani  ya Zanziba iliyowekwa katika Ofisi za makao makuu ya Shirika la ndege la Emirate , wa kwanza kulia ni Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai  , Mhe. Idd Bakari
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Afrika wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu  la Emirates, Badr Abbas kuhusu kuitumia ndege hizo  katika  kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania  mara baada ya kufanyika kwa mkutano  leo katika makao makuu ya Shirika hilo yaliyopo  Dubai,  Wa pili kulia na Meneja wa Masoko wa Afrika wa Shirika hilo.
 Muhamed Riz  akiwa na Balozi Mdogo wa Tanzania,  Dubai, Mhe.  Idd Bakari
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akiagana na  Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Afrika wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu  la Emirates, Badr Abbas mara baada   mkutano uliofanyika baina yao wa kutangaza vivutio vya utalii kupitia ndege za Emirates. Wa pili kulia na Meneja wa Masoko wa Afrika wa Shirika hiloMuhamed Riz  akiwa na Balozi Mdogo wa Tanzania,  Dubai, Mhe. Bakari Iddy
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akikabidhiwa zawadi  na Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Afrika wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu  la Emirates, Badr Abbas mara baada ya kufanyika mkutano  wa  kuitumia ndege za Shirika hilo  katika  kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania  ambapo ndege hizo  hunasafirisha abiria  wapatao  90.2 kwa kila  mwaka, 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akizungmza na  Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Afrika wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu  la Emirates, Badr Abbas mara baada ya kufanyika mkutano  wa  kuitumia ndege za Shirika hilo  katika  kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania  ambapo ndege hizo  hunasafirisha abiria  wapatao  90.2 kwa kila  mwaka, 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Afrika wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu la Emirates, Badr Abbas mara baada mkutano uliofanyika baina yao wa kutangaza vivutio vya utalii kupitia ndege za Emirates. Wa pili kushoto na Meneja wa Masoko wa Afrika wa Shirika hilo Muhamed Riz akiwa na Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai, Mhe. Bakari Iddy
……………………………………………………
Mwandishi Wetu, Dubai.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro amefanya mazungumzo na Uongozi wa juu wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu la Emirates kwa lengo la kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania ambapo vivutio hivyo vya utalii vitaweza kutazamwa na  abiria wapatao  milioni  90.2 ambao husafiri kila  mwaka kwa kutumia ndege hizo
Aidha, Dkt.Ndumbaro amesema  Tangazo hilo litakuwa likitazamwa na mamilioni ya abiria hao kila wakati ndege za Shirika hilo zitakapokuwa zikiruka (take off)
Dkt. Ndumbaro amebainisha hayo leo katika Mji wa Dubai  alipokutana  viongozi wa Shirika hilo ambalo mbali ya kusafirisha abiria milioni 90.2 duniani kote  pia  husafirisha abiria wapatao milioni 20 ambao huunganisha ndege nyingine
Katika hatua nyingine, Dkt.Ndumbaro amesema katika mazungumzo hayo  wamekubaliana  kutaandaliwa makala tano (Documentaries ) za kuelezea vivutio vya utalii vya Tanzania ikiwemo  Zanzibar, Serengeti, Ngorongoro pamoja  na Mlima Kilimanjaro 
” Shirila la ndege la Emirates ni  Shirika kubwa sana Duniani lengo letu kama nchi  ni kuhakikisha abiria wapatao milioni 90.2 wanaviangalia vivutio vyetu kisha wanavipenda halafu wanatembelea Tanzania” amesisitiza Dkt. Ndumbaro
Katika mazungumzo hayo amesema Uongozi wa ndege hizo  umeonesha utayari wa kushirikiana katika kuitangaza Tanzania kiutalii na ifika mwanzoni mwa mwezi wa tano mwaka huu wataingia makubaliano (MOU) baina ya Tanzania na Shirika hilo
Akifafanua mazungumzo hayo Dkt.Ndumbaro amesema kati ya abiria watakaoangalia vivutio wengi wao watavutiwa na hatimaye sehemu ya watu hao waweze  kuja kutembelea  Tanzania 
” Shabaha yetu kubwa kama nchi ni kuhakikisha tunafikia watalii milioni 5 ifikapo mwaka 2025, Tunaamini tutalifikia lengo hilo” amesisitiza Dkt.Ndumbaro
Ameongeza kuwa Tanzania inategemea utalii wake wa Wanyamapori  kwa asilimia 100 hivyo kupitia mkakati wa kutumia wa kutangaza vivutio vingine vya utalii kama vile utalii wa fukwe, utalii wa utamaduni pamoja na utalii wa ikolojia utaweza kujulikana dunia kote na kuwa chachu ya watalii wengi kuanza  kumiminika nchini Tanzania.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Afrika wa Shirika la ndege la Umoja wa Falme za Kiarabu  la Emirates, Badr Abbas amesema Shirika la Emirate lipo tayari kufanya kazi na Tanzania katika kuhakikisha vivutio vya utalii vya Tanzania vinajulikna pande zote za Dunia
” Tutakapofikia makubaliano tutahakikisha pia matangazo ya vivutio vya Utalii wa Tanzania vinawekwa kwenye Tovuti pamoja na mitandao ya kijamii ikiwemo facebook, instagram pamoja na twitter ya Shirika hili ambayo imekuwa ikifuatiliwa na watu wengi Duniani,
Kwa upande wake, Balozi Mdogo wa Dubai, Mhe. Idd Bakari amesema mazungumzo yamekuwa na tija na hivyo kupitia Shirika hilo idadi ya watalii itaongezeka kupitia matangazo yatakayokuwa yakiruka wakati ndege za Shirika hilo zitapokuwa zikiruka
” Mazungumzo haya baina yetu na Shirika la Emirates yataipaisha Tanzania vivutio vya utalii vitaweza kujulikana Duniani kote kuwa vipo Tanzania na hivyo watalii wengi watweza kuitembelea Tanzania 

Katika mazungumzo hayo Ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro pamoja na Balozi Mdogo wa Tanzania, Mhe.Idd Bakari

About the author

mzalendoeditor