| Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Fedha, Bw. Lusius Mwenda, akimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge, kwa uamuzi wa kutoa huduma za uchunguzi wa viashiria vya magonjwa ya moyo pamoja na elimu kuhusu namna ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza kwa Watumishi wa Wizara ya Fedha, katika ukumbi wa Kambarage, jijini Dodoma. |
![]() |
| Baadhi ya viongozi wa Idara, Vitengo na Watumishi wa Wizara ya Fedha, wakipata huduma za vipimo vya viashiria vya magonjwa ya moyo, katika ukumbi wa Kambarage, Wizara ya Fedha, jijini Dodoma. |
![]() |
| Watumishi wa Wizara ya Fedha wakipata huduma za vipimo vya viashiria vya magonjwa yasiyoambukiza, katika ukumbi wa Kambarage, Wizara ya Fedha, jijini Dodoma. |
![]() |
| Watumishi wa Wizara ya Fedha wakipata elimu ya magonjwa yasiyoambukiza, katika ukumbi wa Kambarage, Wizara ya Fedha, jijini Dodoma.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha) |
Na. Peter Haule, WF, Dodoma.
Dkt. Kisenge alisema kuwa utoaji wa elimu kuhusu matumizi ya vyakula vya wanga inapaswa kuzingatia umri na hali ya afya ya mtu, kwani watoto na vijana wengi bado wanahitaji wanga kwa maendeleo yao ya mwili na akili, hususan wale wasiokuwa na changamoto za kiafya.
“Vijana na watoto wanahitaji vyakula vya wanga kwa ajili ya kupata nguvu na kusaidia ukuaji wa akili, upungufu wa wanga unaweza kusababisha watoto kuwa na uwezo mdogo wa kufikiri na kujifunza”, alisema Dkt. Kisenge.
Alisema kuwa mahitaji ya vyakula hubadilika kulingana na umri, akibainisha kuwa watu wenye umri wa zaidi ya miaka 50 wana vihatarishi zaidi vya magonjwa yasiyoambukiza ikilinganishwa na vijana.
Aidha Dkt. Kisenge, alitoa wito kwa Watumishi wa Wizara ya Fedha na watanzania kwa ujumla kula mlo kamili hususani vyakula vya asili zikiwemo mbogamboga na matunda ili kulinda afya za miili yao.
Akieleza kuhusu matumizi ya chumvi alisema kuwa wapo wanaopinga matumizi ya chumvi, alisema chumvi ni muhimu kwa maisha ya binadamu ikitumiwa kwa usahihi.
Vile vile amewataka Watumishi wa Wizara ya Fedha kuepuka matumizi ya yaliyopita kiasi ya pombe, vinywaji vinavyoongeza nguvu na kufanya kazi kupita kiasi, ametoa wito wa kupata mlo kamili, kufanya mazoezi na kuwa na utamaduni wa kupima afya.
Alisema kuwa utamaduni wa kupima afya unasaidia kupunguza gharama kubwa za matibabu na pia kumfanya mtumishi kuendelea kutoa huduma kwa wananchi kwa ufanisi.
Alibainisha kuwa watumishi wa Wizara ya Fedha watatumia vizuri elimu waliyoipata kuhusu mtindo bora wa maisha, lishe sahihi na umuhimu wa kufanya mazoezi, ili kuwa na afya njema itakayosaidia kutoa huduma kwa watanzania kwa ufanisi.









