Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Herman Kasekende, wakisaini Mkataba wa kugharamia ukamilishaji wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu (loti 3) na cha nne (loti 4) kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi Isaka, yenye thamani ya takriban dola za Marekani bilioni 1.277, hafla iliyofanyika leo Aprili 28,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Herman Kasekende, wakionesha Mkataba wa kugharamia ukamilishaji wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu (loti 3) na cha nne (loti 4) kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi Isaka, yenye thamani ya takriban dola za Marekani bilioni 1.277, hafla iliyofanyika leo Aprili 28,2026 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Herman Kasekende, wakibadilishana Mkataba wa kugharamia ukamilishaji wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu (loti 3) na cha nne (loti 4) kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi Isaka, yenye thamani ya takriban dola za Marekani bilioni 1.277, hafla iliyofanyika leo Aprili 28,2026 jijini Dodoma.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa Mkataba wa kugharamia ukamilishaji wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu (loti 3) na cha nne (loti 4) kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi Isaka, yenye thamani ya takriban dola za Marekani bilioni 1.277, hafla iliyofanyika leo Aprili 28,2026 jijini Dodoma.

Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Mb), akizungumza mafanikio ya Reli ya Kisasa wakati wa hafla ya utiaji saini wa Mkataba wa kugharamia ukamilishaji wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu (loti 3) na cha nne (loti 4) kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi Isaka, yenye thamani ya takriban dola za Marekani bilioni 1.277, hafla iliyofanyika leo Aprili 28,2026 jijini Dodoma.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar.Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa , Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mhe. Sulemani Kakoso,Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba na Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Walter Kahyarara, wakiwa katika picha ya pamoja na mabalozi wa Sweden, Italy na Poland baada ya hafla ya utiaji saini wa Mkataba wa kugharamia ukamilishaji wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu (loti 3) na cha nne (loti 4) kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi Isaka, yenye thamani ya takriban dola za Marekani bilioni 1.277, hafla iliyofanyika leo Aprili 28,2026 jijini Dodoma.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF – Dodoma)
Na.Alex Sonna,Mzalendo blog-DODOMA
Serikali imepiga hatua nyingine kubwa katika ujenzi wa uchumi wa kisasa baada ya kusaini mkataba wa ufadhili wa takribani dola za Marekani bilioni 1.277 kwa ajili ya kuendeleza mradi wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu na cha nne kutoka Makutupora mkoani Singida hadi Isaka.
Mkataba huo umesainiwa leo Aprili 28, 2026 jijini Dodoma,Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, alisaini kwa niaba ya Serikali huku Benki ya Standard Chartered ikiwakilishwa na Afisa Mtendaji Mkuu wake, Bw. Herman Kasekende.
Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Musa Omar,amesema kuwa fedha hizo ni sehemu ya jumla ya dola bilioni 2.33 zinazotarajiwa kugharamia utekelezaji wa mradi huo mkubwa wa kimkakati.
Ameeleza kuwa ufadhili huo unatokana na ushirikiano wa kimataifa unaohusisha taasisi za dhamana za mikopo ya mauzo ya nje kutoka Italia (SACE), Sweden (EKN) na Poland (KUKE), chini ya uratibu wa Benki ya Standard Chartered.
“Mradi huu ni uti wa mgongo wa mageuzi ya uchumi wa Tanzania. Unalenga kuunganisha Bandari ya Dar es Salaam na ukanda wa Ziwa pamoja na nchi jirani, hivyo kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara na usafirishaji katika Afrika Mashariki na Kati,” amesema Waziri Omar.
Ameongeza kuwa SGR siyo tu uwekezaji wa miundombinu bali ni dira ya maendeleo ya muda mrefu inayolenga kuchochea ukuaji wa uchumi, kuongeza ajira na kuimarisha ushindani wa taifa katika soko la kimataifa.
Kwa upande wake, Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amesema mradi huo utakapokamilika utaongeza uwezo wa kusafirisha hadi tani milioni tano za mizigo kwa mwaka, huku ukipunguza kwa kiasi kikubwa muda wa usafirishaji na gharama zake.
Prof.Mbarawa amefafanua kuwa tayari huduma za SGR kati ya Dar es Salaam na Dodoma zimeanza kuonyesha mafanikio makubwa, zikiwa zimesafirisha takriban abiria milioni sita na tani zaidi ya 120,000 za mizigo.
“Mbali na kupunguza muda wa safari kutoka saa 12 hadi saa 3, mradi huu umechangia pia kupunguza matumizi ya mafuta kwa zaidi ya lita milioni 17 na kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa kwa zaidi ya asilimia 50,” amesisitiza Prof. Mbarawa.
Aidha, amebainisha kuwa upanuzi wa reli hiyo hadi Isaka utafungua fursa mpya za biashara kwa nchi za jirani, kupunguza gharama za usafirishaji na kuimarisha ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la kikanda na kimataifa.
Nao Mabalozi wa nchi za Sweden, Mhe. Charlotta Marcias, Balozi wa Italia, Mhe. Giuseppe Sean Coppola na Mwakilishi wa Balozi wa Poland nchini, Bw. Sergiusz Wolski, walioshuhudia hafla hiyo wameeleza kuridhishwa kwao na maendeleo ya mradi wa SGR, wakisisitiza kuwa ni ishara ya ushirikiano imara wa kiuchumi na kidiplomasia kati ya Tanzania na mataifa yao.
Waliongeza kuwa mafanikio yaliyopatikana katika awamu zilizopita yamefungua milango kwa uwekezaji zaidi, huku wakiahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika miradi mikubwa ya maendeleo inayozingatia viwango vya kimataifa na uendelevu wa mazingira.