Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akichangia mjadala kufuatia taarifa ya Kamisheni ya Umoja wa Mataifa inayosimamia Uchumi Afrika (UNECA), iliyochambua athari za mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati namna ulivyoleta athari hasi za kiuchumi na kijamii katika Bara la Afrika na namna ya kukabiliana nazo, katika Mkutano wa 58 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi na Magavana wa Benki Kuu wa Afrika, unaofanyika jijini Tangier nchini Morocco.

Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akishiriki Mkutano wa 58 wa Mawaziri wa Fedha, Mipango na Maendeleo ya Uchumi na Magavana wa Benki Kuu wa Afrika wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa inayosimamia Uchumi Afrika (UNECA), unaofanyika jijini Tangier nchini Morocco.
ambao pamoja na mambo mengine unajadili athari za mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati namna ulivyoleta athari hasi za kiuchumi na kijamii katika Bara la Afrika na namna ya kukabiliana nazo. Mkutano huo umewashirikisha pia Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji Mhe. Dkt. Pius Chaya na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha, Tangier, Morocco)