Featured Kitaifa

UTUMISHI NA e-GA WAJIPANGA KUTUMIA MIFUMO KURAHISISHA UTENDAJI KAZI

Written by mzalendoeditor

 

 Afisa TEHAMA kutoka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw.Hossea Laizek,akizungumza na waandishi wa habari kwenye banda la e-GA wakati wa kilele cha Maonesho ya wiki ya ubunifu 2023 yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia yaliyomalizika leo Aprili 28,2023 kwenye  uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Afisa TEHAMA  kutoka  Mamkala Mtandao (e-GA)  Tumaini Masinsi ,akizungumza na waandishi wa habari kwenye banda la e-GA wakati wa kilele cha Maonesho ya wiki ya ubunifu 2023 yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia yaliyomalizika leo Aprili 28,2023 kwenye  uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Afisa TEHAMA kutoka Mamlaka Mtandao Vannesa Mhando  ,akizungumza na waandishi wa habari kwenye banda la e-GA wakati wa kilele cha Maonesho ya wiki ya ubunifu 2023 yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia yaliyomalizika leo Aprili 28,2023 kwenye  uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

,WANANCHI wakipata elimu kwenye banda la e-GA wakati wa kilele cha Maonesho ya wiki ya ubunifu 2023 yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia yaliyomalizika leo Aprili 28,2023 kwenye  uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Na.Bolgas Odilo-DODOMA

Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora  kwa kushirikiana na Mamlaka ya Serikali Mtandao ( e-GA) imejipanga kutumia mifumo ya teknolojia kurahishisha utendaji kazi wa watumishi wa umma.

Hayo yameelezwa leo Aprili 28,2023 Jijini Dodoma na Afisa TEHAMA kutoka Utumishi Bw.Hossea Laizek,akizungumza na waandishi wa habari kwenye banda la e-GA wakati wa kilele cha Maonesho ya wiki ya ubunifu 2023 yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia yaliyomalizika leo Aprili 28,2023 kwenye  uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Amesema kupitia mfumo wa E mrejesho watumishi  wanaweza kufuatilia taarifa mbalimbali kuhusu malalamiko,pongezi na huduma mbalimbali zinazotolewa katika ofisi.

Pia amesema  kuna mfumo wa watumishi porto ambao unaweza   kuwahudumia watumishi wa uuma bila ya kufika katika kituo cha kazi ikiwa ni pamoja na kufanya uhamisho.

“Kuna huduma nyingine inawezesha watumishi kupanga plan zao za mwaka na kurekodi utendaji kazi wake wa kazi,”amesema Laizek

Kwa upande wake Afisa TEHAMA  kutoka  Mamkala Mtandao (e-GA)  Tumaini Masinsi amesema kupitia maonesho hayo kuna  mfumo uitwao Oxgen Net ambao ni wa Whatsup ya ndani.

“Oxgen ni chatting platform ni ya hapa ndani kwa ajili ya kuchat na kwa ajili ya video Call na kwa ajili ya kujifunza vitu mbalimbali.Namna ya kuipata unaweza kutumia Web Oxgen Net na kuitumia na katika  Playstore,”amesema

Amesema katika maonesho hayo  wamekuja na bunifu mbalimbali za mfumo kwenye mambo ya tehama ambazo zimefanywa na vijana wabunifu  wazalengo.

“Tuna bunifu mbalimbali ambazo zimefanya na wabunifu wazalendo kwa ajili ya kurahisisha vikao vya madaniwani na Halmashauri  ikiwa ni pamoja na kuweka vizuri agenda,”amesema

Pia amesema wana E dodoso  imetengezwa kwa ajili ya watafiti kukusanya data na kuchakata   ambazo zitarahishisha uandishi wa ripoti mbalimbali.

Naye,Afisa TEHAMA kutoka Mamlaka Mtandao Vannesa Mhando  amesema wao kama vijana wanajifunza uzalendo na kutiwa moyo kuendelea kutengeneza suluhu ambazo zitatua matatizo ya watanzania.

Amesema wanajiendeleza kiteknolojia kwa ajili ya kukuza ujuzi na kuendeleza mambo mazuri.

“Mfano kama siku ya leo tumeonesha suluhu mbalimbali za mifumo ambayo itapunguza gharama kubwa na kubwa kuliko yote imefanywa na sisi wazawa,”amesema.

About the author

mzalendoeditor