Featured Michezo

YANGA YATUPWA TUNISIA KOMBE LA SHIRIKISHO

Written by mzalendoeditor
KLABU ya Yanga itakutana na Club Africain ya Tunisia katika mechi ya mchujo wa kuwania kucheza Hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Katika droo iliyopangwa leo makao makuu ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Yanga itaanzia nyumbani Novemba 2, kabla ya kucheza mechi ya marudiano Tunisia Novemba 9. 
Yanga wamepangwa na klabu hiyo baada ya kutolewa na Klabu ya Al Hilal ya Sudan kwa jumla ya mabao 2-1, wakitoa suluhu ya 1-1 katika mchezo wa kwanza uliochezwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam na kupoteza kwa bao 1-0 katika maechi ya marudiano iliyochezwa jijini Kharthoum.
Club Africain inakutana na Yanga, ikiwa na rekodi ya kuitoa Klabu ya Kipanga ya visiwani Zanzibar kwa jumla ya mabao 7-0, wakitoka suluhu katika mchezo wa kwanza uliochezwa nchini Tanzania na kuifunga 7-0 katika mchezo wa marudiano uliopigwa nchini Tunisia.

About the author

mzalendoeditor