Featured Kitaifa

RAIS RUTO ATANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI

Written by mzalendoeditor

Nairobi, Kenya

Rais wa Kenya William Ruto ametangaza Baraza lake la kwanza la Mawaziri saa chache baada ya kufanya kikao na Baraza la Mawaziri waliohudumu chini ya Utawala wa Serikali ya Uhuru Kenyatta.

Taarifa zimesema, katika Baraza hilo, Ruto amemteua Kiongozi wa Chama cha Amani National Congress, Musalia Mudavadi kuwa Waziri Kiongozi. 

Mudavadi atamsaidia Rais na Naibu Rais, Rigathi Gachagua kufuatilia shughuli katika wizara za Serikali.

Wengine aliowateua katika Baraza hilo ni;

1. Waziri wa Usalama wa Ndani – Prof Kithure Kindiki

2. Waziri wa Masuala ya Kigeni – Dkt Alfred Mutua

3. Waziri wa Elimu – Ezekiel Machogu

4. Waziri wa Kawi – Davis Chirchir

5. Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki – Rebecca Miano

6. Waziri wa Ulinzi – Aden Duale

7. Waziri wa Utalii – Penina Malonza

8. Waziri wa Afya – Susan Nakumicha Wafula

9. Waziri wa Michezo – Ababu Namwamba

10. Waziri wa Ardhi – Zacharia Mwangi Njeru

11. Waziri wa Leba – Florence Bore

12. Waziri wa Biashara – Moses Kuria

13. Waziri wa Maji – Alice Wahome

14. Waziri wa Mazingira – Roselinda Soipan Tuya

15. Waziri wa Fedha – Profesa Njuguna Ndung’u

16. Waziri wa Habari na Mawasiliano – Eliud Owalo

17. Waziri wa Kilimo – Franklin Mithika Linturi

18. Waziri wa Huduma za Umma, Jinsia na Usawazishaji – Aisha Jumwa

19. Waziri wa Barabara – Kipchumba Murkomen

20. Waziri wa Sekta ya Biashara Ndogo na za Wastani (SMEs) – Simon Chelugui

21. Waziri wa Uchimbaji Madini – Salim Mvurya

22. Mshauri wa Shirika la Masuala ya Wanawake – Harriet Chigai

23. Mshauri wa Masuala ya Usalama wa Ndani – Monica Juma

24. Mwanasheria Mkuu – Justin Muturi

25. Katibu katika Baraza la Mawaziri – Mercy Wanja.

About the author

mzalendoeditor