Featured Kitaifa

RAIS SAMIA APOKEA HATI YA UTAMBULISHO WA BALOZI WA MALAWI,ASHIRIKI MKUTANO WA EAC KWA NJIA YA MTANDAO,IKULU CHAMWINO

Written by mzalendoeditor

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Balozi wa Jamhuri ya Malawi hapa nchini Mhe. Andrew Posyantos Efron Zumbe kabla ya kupokea Hati yake ya Utambulisho katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino, Jijini Dodoma leo tarehe 29 Machi, 2022.

Balozi wa Jamhuri ya Malawi hapa nchini Mhe. Andrew Posyantos Efron Zumbe akiwasilisha Hati yake ya Utambulisho katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino, Jijini Dodoma leo tarehe 29 Machi, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Malawi hapa nchini Mhe. Andrew Posyantos Efron Zumbe mara baada ya kupokea Hati yake ya Utambulisho katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino, Jijini Dodoma leo tarehe 29 Machi, 2022.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Malawi hapa nchini Mhe. Andrew Posyantos Efron Zumbe mara baada ya mazungumzo yao Ikulu Jijini Dodoma leo tarehe 29 Machi, 2022.





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akishiriki Mkutano wa 19 wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) uliofanyika kwa njia ya Mtandao, Ikulu Chamwino Jijini Dodoma leo tarehe 29 Machi, 2022.

About the author

mzalendoeditor