Mgombea wa Nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Wakulima (AAFP), Kunje Ngombale Mwiru,akipokea Begi lenye Fomu za kugombea nafasi ya Rais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele katika Ofisi za Tume hiyo Njedengwa Jijini Dodoma tarehe 09 Agosti, 2025. Kushoto ni Mgombea Mwenza Chumu Abdallah Juma.
Mgombea wa Nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Wakulima (AAFP), Kunje Ngombale Mwiru, akionesha Begi lenye Fomu zake za kugombea nafasi hiyo mara baada ya kukabidhiwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele katika Ofisi za Tume hiyo Njedengwa Jijini Dodoma tarehe 09 Agosti, 2025.
Na.Alex Sonna-DODOMA
MGOMBEA wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Wakulima (AAFP), Kunje Ngombale Mwiru, pamoja na mgombea mwenza wake, Chumu Abdallah Juma, wamekabidhiwa fomu ya uteuzi wa kugombea nafasi hiyo katika Makao Makuu ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) jijini Dodoma.
“Serikali yangu itakuwa ya mchakamchaka yenye vipaumbele vitatu; cha kwanza ni uzalendo, pili uzalendo, na cha tatu ni uzalendo kwa taifa letu.”