Featured Kitaifa

MKUTANO MKUU WA SABA WA CWT KUFANYIKA MEI 28 NA 29,MWAKA HUU JIJINI DODOMA

Written by mzalendoeditor

TAARIFA KWA UMMA

Ofisi ya Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) inapenda kuwataarifu walimu na Watanzania wote kwa ujumla kuwa chama kinatarajia kufanya Mkutano mkuu wa saba utakaofanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia 28 na 29 Mei Jijini Dodoma. 

Pamoja na mambo mengine Mkutano Mkuu huo utafanya uchaguzi wa viongozi kwa nafasi mbalimbali kwa Ngazi ya Taifa 

Hii ni baada ya kukamilika kwa chaguzi zilizokuwa zikiendelea nchini kote kwa ngazi za shule (Tawi), Wilaya na Mikoa na sasa chama kitakamilisha Ngazi ya Taifa. 

Miongoni mwa nafasi za kitaifa zinazotarajiwa kufanyiwa uchaguzi ni pamoja na:-

i.Rais wa CWT 

ii.Makamu wa rais CWT

iii. Katibu Mkuu wa CWT 

Iv.  Naibu katibu mkuu CWT

V.Mweka hazina CWT 

Vi. Mwakilishi wa walimu wenye ulemavu 

vii. Mwakilishi wa walimu vijana

Viii. Mwakilishi wa Walimu wanawake 

ix.Mjumbe wa kamati ya utendaji TUCTA kutoka CWT

x.Wadhamini watatu

Xi. Vitengo mbalimbali vya chama

Chama kinawakaribisha wajumbe wa mkutano mkuu kushiriki tukio lao hilo muhimu na la kihistoria 

Aidha orodha ya wagombea wa nafasi imetolewa kwa Umma.

Imetolewa na 

JUMA A. DEDU – AFISA HABARI NA MAHUSIANO CWT HQ

About the author

mzalendoeditor