Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, akiagana na Kiongozi wa Timu ya wataalamu kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Nicolas Blancher, baada ya kufungua kikao kikao cha Timu ya Wataalamu wa Wizara ya Fedha na wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma, ambacho kitajadili tathmini katika program mbalimbali zinazofadhiliwa na IMF nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, akizungumza wakati akifungua kikao cha Timu ya Wataalamu wa Wizara ya Fedha na wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), ukiongozwa na Bw. Nicolas Blancher (hayupo pichani), kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma, ambacho kitajadili tathmini katika program mbalimbali zinazofadhiliwa na IMF nchini.

Kiongozi wa Timu ya wataalamu kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Nicolas Blancher, akizungumza wakati wa kikao cha Timu ya Wataalamu wa Wizara ya Fedha na wa IMF, kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma, ambacho kilijadili tathmini ya program mbalimbali zinazofadhiliwa na IMF nchini

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, akifafanua jambo wakati wa kikao cha Timu ya Wataalamu wa Wizara ya Fedha na wa IMF, kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma, ambacho kinajadili tathmini katika program mbalimbali zinazofadhiliwa na IMF nchini.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, akiongoza kikao cha Timu ya Wataalamu wa Wizara ya Fedha na wa IMF, kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma, ambacho kinajadili tathmini katika program mbalimbali zinazofadhiliwa na IMF nchini.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, na Kiongozi wa Timu ya wataalamu kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Nicolas Blancher, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufungua wakati wa kikao cha Timu ya Wataalamu wa Wizara ya Fedha na wa IMF, kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma, ambacho kilijadili tathmini katika program mbalimbali zinazofadhiliwa na IMF nchini. Kutoka kulia ni Kaimu Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bw. Rished Bade na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba. Kushoto ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Sebastian Acevedo.

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, akiteta jambo na Kiongozi wa Timu ya wataalamu kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Nicolas Blancher, baada ya kikao cha Timu ya Wataalamu wa Wizara ya Fedha na wa IMF, kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma, ambacho kinajadili tathmini katika program mbalimbali zinazofadhiliwa na IMF nchini.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dodoma)
Na. Joseph Mahumi na Saidina Msangi, WF, Dodoma
Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, limeipongeza Tanzania kwa ushirikiano mzuri uliopo kati yake na Shirika hilo katika utekelezaji na usimamizi wa mageuzi ya kiuchumi chini ya programu za Extended Credit Facility-(ECF), inayohusisha upatikanaji wa mkopo nafuu kwa ajili ya kuimarisha uchumi wa nchi kupitia sekta za uzalishaji na huduma za jamii na Resilience Sustainability Facility (RSF) ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Pongezi hizo zimetolewa na Kiongozi wa Timu ya Wataalamu kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Nicolas Blancher, wakati alipoongoza timu ya wataalamu kutoka Shirika hilo iliyofika kufanya tathmini ya kina ya program mbalimbali inayofadhili nchini, katika kikao na Ujumbe wa Tanzania ukioongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Bw. Blancher amesema kuwa dhamira ya IMF ni kuendelea kuunga mkono jitihada za Tanzania katika kukamilisha programu zilizopo (ECF na RSF) na kupanga hatua zinazofuata katika programu hizo.
“Moja ya lengo kuu la ziara hii ya wiki mbili ni kujadili masuala ya msingi ya sera za uchumi, hususan namna ambavyo Tanzania inakabiliana na changamoto za mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati” alisema Bw. Blancher.
Aidha, aliongeza kuwa Tanzania iendelee kuimarisha zaidi sekta ya fedha, kuongeza matumizi ya kijamii katika sekta za afya na elimu, ili kuchochea ukuaji wa sekta binafsi na ajira, sambamba na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Fedha ambaye pia ni Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, amelishukuru Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF kwa ushirikiano wake endelevu katika kusaidia utekelezaji wa mageuzi ya kiuchumi nchini.
Dkt. Mwamba alisisitiza dhamira ya Serikali kuendelea kushirikiana kwa karibu na IMF ili kufikia malengo ya ukuaji jumuishi na maendeleo endelevu na Serikali ina matumaini ya kufikia makubaliano yatakayowezesha upatikanaji wa rasilimali fedha kwa wakati na kuimarisha uchumi wa Taifa.
“Katika tathmini ya utekelezaji wa programu ya ECF, vigezo viwili kati ya nane vilivyokuwa vinatarajiwa vimekamilika, ikiwemo kuandaliwa kwa mfumo wa msaada wa ukwasi kwa dharura (ELA) na maboresho ya mfumo wa dhamana kwa taasisi za fedha, na vigezo vitano vinaendelea kutekelezwa, ikiwemo maboresho ya sheria ya mipango ya uwekezaji wa umma, uboreshaji wa mifumo ya marejesho ya VAT, na muswada wa sheria ya dhamana unaolenga kupanua wigo wa mali zinazoweza kutumika kama dhamana” alisema Dkt. Mwamba.
Aliongeza kuwa, kwa upande wa Programu ya RSF, hatua tano kati ya nane zimekamilika, zikiwemo mipango ya muda mrefu ya sekta ya nishati inayozingatia mabadiliko ya tabianchi, pamoja na uanzishwaji wa mifumo ya ukusanyaji wa takwimu za athari za tabianchi katika sekta ya fedha.