Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Kulia), akisalimiana na Mkurugenzi Mpya wa Benki ya Afrexim Kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Humphrey Nwugo, aliyefika kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni, akiambatana na wajumbe wengine wa benki hiyo, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo alitumia fursa hiyo kuelezea umuhimu wa ushirikiano imara, mitaji ya muda mrefu na mbinu bunifu za ufadhili kati ya Benki hiyo na Serikali ya Tanzania ili kufikia azma ya kuwa uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050.

Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Kushoto), akibadilishana kadi na Mkurugenzi Mpya wa Benki ya Afrexim Kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Humphrey Nwugo, aliyefika kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni, akiambatana na wajumbe wengine wa benki hiyo, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo alitumia fursa hiyo kuelezea umuhimu wa ushirikiano imara, mitaji ya muda mrefu na mbinu bunifu za ufadhili kati ya Benki hiyo na Serikali ya Tanzania ili kufikia azma ya kuwa uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050.

Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (katikati), akiongoza kikao chake na Ujumbe wa Benki ya Afrexim ukiongozwa na Mkurugenzi wake Mpya wa Kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Humphrey Nwugo, aliyefika kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni, kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo alitumia fursa hiyo kuelezea umuhimu wa ushirikiano imara, mitaji ya muda mrefu na mbinu bunifu za ufadhili kati ya Benki hiyo na Serikali ya Tanzania ili kufikia azma ya kuwa uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050.

Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati wa kikao chake na Ujumbe wa Benki ya Afrexim ukiongozwa na Mkurugenzi wake Mpya wa Kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Humphrey Nwugo (hayupo pichani), aliyefika kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni, kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo alitumia fursa hiyo kuelezea umuhimu wa ushirikiano imara, mitaji ya muda mrefu na mbinu bunifu za ufadhili kati ya Benki hiyo na Serikali ya Tanzania ili kufikia azma ya kuwa uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi Mpya wa Benki ya Afrexim Kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Humphrey Nwugo, baada ya kikao cha Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), na ujumbe wa Benki hiyo, wakati Mkurugenzi huyo alipofika kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni, kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Katikati), Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (wa tatu kulia), Mkurugenzi Mpya wa Benki ya Afrexim Kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Humphrey Nwugo (wa tatu kushoto), na maafisa wengine waandamizi wa Wizara ya Fedha na Benki ya Afrexim, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dar es Salaam)
Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam
Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amesema Tanzania inaiona Benki ya Afrexim kama mshirika wa kimkakati katika safari ya mageuzi ya kiuchumi ya nchi, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano imara, mitaji ya muda mrefu na mbinu bunifu za ufadhili ili kufikia azma ya kuwa uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050.
Akizungumza Dar es Salaam wakati wa kikao na ujumbe wa Afreximbank ulioongozwa na Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Benki hiyo, Bw. Humphrey Nwugo, aliyefika kujitambulisha baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni, Balozi Omar alimkaribisha rasmi na kumpongeza kwa uteuzi wake mpya, akieleza matumaini ya Tanzania kuimarisha zaidi uhusiano wa muda mrefu kati ya Tanzania na taasisi hiyo ya kifedha ya Afrika.
Alisema kwa miaka mingi Afreximbank imeendelea kuwa miongoni mwa taasisi muhimu za kifedha barani Afrika, huku Tanzania ikiwa sehemu ya safari hiyo na kwamba Serikali inathamini mchango wa benki hiyo katika kusaidia biashara, miundombinu, ukuaji wa viwanda na maendeleo ya sekta binafsi.
Mhe. Balozi Omar alisema kuwa, Tanzania imefarijika na dhamira ya Afreximbank ya kuhamasisha dola za Marekani bilioni moja zaidi ndani ya miezi 12 ijayo kwa ajili ya uwekezaji nchini, hasa katika sekta za viwanda, miundombinu na biashara ndogo na za kati.
Aidha, alisema utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 pamoja na Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Miaka Mitano unalenga kujenga uchumi shindani unaoongozwa na sekta binafsi na kwamba ili kufikia lengo hilo kutahitaji ubia madhubuti, uwekezaji wa muda mrefu na ushirikiano wa karibu na taasisi kama Afreximbank.
Alibainisha kuwa pamoja na mafanikio yaliyopo, bado kuna nafasi kubwa ya kupanua ushirikiano katika maeneo ya kimkakati yakiwemo miundombinu, viwanda, afya na uwezeshaji wa biashara. Aliongeza kuwa kikao hicho ni fursa muhimu ya kubadilishana mawazo kuhusu maeneo ya maslahi ya pamoja na kutafuta njia za vitendo za kuimarisha ushirikiano huo.
Alitaja maeneo yanayohitaji msukumo zaidi kuwa ni kusaidia ukuaji wa viwanda, kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi, kuendeleza mtaji watu na kuongeza ushindani wa biashara ya Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Benki ya Afriexim, Bw. Humphrey Nwugo, aliipongeza Tanzania kwa hatua kubwa iliyopiga kiuchumi na kuaghidi kuwa Benki yake iko tayari kuendeleza ushirikiano wa muda mrefu ili kufikia matarajio yake ya agenda ya kufikia uchumi wa dola za Marekani trilioni moja kupitia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
Alisema kuwa Afriexim ina nia ya kuwekeza kwenye miradi ya kimkakati ikiwemo mafuta, madini, chuma, magadi na imejipanga kuendelea kuisaidia sekta binafsi kwa kuipatia mikopo na mitaji ili iweze kuchangia katika kuwekeza kwenye sekta zitakazochochea zaidi ukuaji wa uchumi ikiwemo uongezaji wa thamani ya bidhaa.
Benki ya Afrexim imeendelea kuwa mshirika muhimu wa Tanzania katika kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo, ikitoa fedha na dhamana zenye thamani ya mabilioni ya dola za Marekani kwa ajili ya miundombinu, sekta ya fedha na miradi ya kimkakati.
Mwaka 2018 Benki ya Afrexim ilitoa dhamana yenye thamani ya dola za Marekani milioni 800 kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa Julius Nyerere katika bonde la Rufiji, hatua iliyowawezesha wakandarasi kutoka Misri kutekeleza mradi huo.
Mbali na hilo, benki hiyo imetoa jumla ya dola za Marekani milioni 700 kusaidia miradi mbalimbali ya miundombinu, ikiwemo sehemu za kwanza hadi za nne za reli ya kisasa ya SGR.
Katika sekta ya fedha, Benki ya Afrexim imeidhinisha jumla ya dola za Marekani milioni 230 kwa mabenki ya biashara nchini Tanzania. Vilevile, imewezesha sekta binafsi kwa kutoa mikopo na huduma za kifedha zenye thamani ya dola za Marekani milioni 80.