Featured Kitaifa

BALOZI NCHIMBI AWASILI SONGEA MAZISHI YA MZEE SONGAMBELE

Written by mzalendoeditor

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Songea, mkoani Ruvuma na kupokelewa na viongozi wa Chama na Serikali mkoani humo, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed na Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma, Mohamed Ali Khalfan, leo Jumatatu tarehe 2 Juni 2025.

Balozi Nchimbi amewasili mjini Songea, kwa ajili ya kushiriki mazishi ya mwanasiasa mkongwe na mmoja wa wapigania uhuru wa Tanganyika, na waasisi wa Chama cha TANU na CCM, Alhaj Mzee Mustafa Mohamed Songambele, aliyefariki usiku wa kuamkia Juni 1, 2025 jijini Dar es Salaam na kutarajiwa kuzikwa leo mjini Songea.    

About the author

mzalendoeditor