Featured Kitaifa

DKT.JAFO ATAKA WATANZANIA KUNUNUA MABATI YANAYOZALISHWA NCHINI

Written by mzalendoeditor
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akikagua shughuli mbalimbali  za uzalishaji wa Mabati katika  Kiwanda Cha  ALAF kilichopo Jijini Dodoma,mara baada ya ziara yake ya kukagua utendaji kazi wa kiwanda hicho leo Aprili 22,2025.
Na Alex Sonna-DODOMA
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo amesema Serikali  imeweka utaratibu mzuri wa kuvilinda Viwanda vya mabati nchini kwa kuweka kodi kubwa kwa mabati yanayotoka nje ya Nchi huku akiwataka  Watanzania kununua mabati yanayozalishwa na Viwanda nchini.
Dkt.Jafo ameyasema hayo leo  Aprili 22,2025,  mara baada ya ziara ya kukagua shughuli za uzalishaji wa Kiwanda cha mabati Cha  ALAF  Jijini Dodoma ambapo amesema kuwa  kiwanda hicho uzalishaji wake umekuwa ukiongezeka kila siku.
Waziri Jafo amesema Kiwanda hicho ni cha kihistoria kwani kipo nchini tangu mwaka 1960 na kina share na Serikali kwa asilimia 24.
Amesema Kiwanda hicho kwa  sasa kinauwezo  wa kuzalisha bati  ya rangi nyeupe tani 100,000 na za rangi tani 75,000 kuanzia geji 22 hadi 32 kulingana na mahitaji husika hali inayochangia nchi kujitosheleza kwa bidhaa hiyo ya mabati.
“Maana yake tuna kila sababu ya kuweka mikakati ya kuzuia uingizaji wa mabati kutoka nje ili kulinda ajira zetu,”amesema Waziri Jafo
Amesema wanapoenda katika mchakato wa bajeti lazima waangalie  mikakati ya bati kutoka nje kwa kuweka kodi ya kutosha ili ya ndani yaweze kuzalishwa na kupata soko
“Kwa sababu lazima tuvilinde Viwanda vya ndani.Nafahamu mmeajiri zaidi ya watu 500,  niwahakikishie Serikali itaendelea kuwalinda ila niwaombe Watanzania tununue bati za ndani,”amesema Waziri Jafo.
Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi,Sekta ya uwekezaji Viwanda na Biashara Jiji la Dodoma. Bi.Mwajabu  Nyamkomola  ameziomba Halmashauri zote nchini kutumia mabati ya Alaf katika ujenzi wa vitu mbalimbali ikiwemo Zahanati na vituo vya Afya.
“Tumeona ubora wa vitu vilivyozungumzwa wakiwepo TBS  wanahakikisha wanapata bidhaa zenye ubora wa hali ya juu na utaendelea kuhakikisha hivi Viwanda havipati vikwazo vyovyote bali wanazidi kusonga mbele ,”amesema Bi. Nyamkomola
Naye Meneja Uhusiano wa ALAF Bi.Hawa Bayumi,amesema katika kipindi cha mwaka mmoja Alaf inazalisha bati za rangi hapa hapa nchini na wanauwezo wa kuhudumia wateja wao kwa wakati.
“Sio tu tunaweza kuzalisha nchini lakini pia kumhakikishia huyu mlaji anapata bidhaa ambazo ni za Viwango na zitadumu miaka na miaka tunawakaribisha sana Watanzania waweze kutumia bidhaa zetu pamoja na kupenda bidhaa zetu,watanzania tupende vitu vya kwetu kwa sababu faida inaenda kwa watoto wetu na kwenye gawio la Serikali
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akikagua shughuli mbalimbali  za uzalishaji wa Mabati katika  Kiwanda Cha  ALAF kilichopo Jijini Dodoma,mara baada ya ziara yake ya kukagua utendaji kazi wa kiwanda hicho leo Aprili 22,2025.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akikagua shughuli mbalimbali  za uzalishaji wa Mabati katika  Kiwanda Cha  ALAF kilichopo Jijini Dodoma,mara baada ya ziara yake ya kukagua utendaji kazi wa kiwanda hicho leo Aprili 22,2025.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akipata maelezo mara baada ya kufanya ziara ya kukagua  shughuli mbalimbali  za uzalishaji wa Mabati katika  Kiwanda Cha  ALAF kilichopo Jijini Dodoma, leo Aprili 22,2025.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akikagua shughuli mbalimbali  za uzalishaji wa Mabati katika  Kiwanda Cha  ALAF kilichopo Jijini Dodoma,mara baada ya ziara yake ya kukagua utendaji kazi wa kiwanda hicho leo Aprili 22,2025.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akikagua shughuli mbalimbali  za uzalishaji wa Mabati katika  Kiwanda Cha  ALAF kilichopo Jijini Dodoma,mara baada ya ziara yake ya kukagua utendaji kazi wa kiwanda hicho leo Aprili 22,2025.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Dkt.Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukagua  shughuli mbalimbali  za uzalishaji wa Mabati katika  Kiwanda Cha  ALAF kilichopo Jijini Dodoma,leo Aprili 22,2025.

About the author

mzalendoeditor