Featured Michezo

BARRICK NORTH MARA KIDEDEA MECHI YA SOKA YA KIRAFIKI NA TIMU YA CHUO CHA MWALIMU NYERERE

Written by mzalendoeditor
Wachezaji wa timu ya Barrick North Mara na Chuo kikuu cha Mwalimu Nyerere wakipata mawaidha kabla ya kuanza mechi ya soka ya kirafiki iliyofanyika katika viwanja vya North Mara ambapo North Mara iliibuka na ushindi wa bao 1-0
Kikosi cha timu ya Barrick North Mara katika picha ya pamoja kabla ya mchezo wa soka wa kirafiki na timu ya iliyofanyika katika viwanja vya North Mara ambapo North Mara iliibuka na ushindi wa bao 1-0
Wachezaji wa timu ya Barrick North Mara wakifanya mazoezi kabla ya kuanza mechi ya soka ya kirafiki iliyofanyika katika viwanja vya North Mara ambapo North Mara iliibuka na ushindi wa bao 1-0
Wachezaji wa timu ya Barrick North Mara na Chuo kikuu cha Mwalimu Nyerere wakipambana vikali uwanjani wakati wa mechi ya soka ya kirafiki iliyofanyika katika viwanja vya North Mara ambapo North Mara iliibuka na ushindi wa bao 1-0
***
Timu ya soka ya wafanyakazi wa mgodi wa Barrick North Mara uliopo wilayani Tarime mkoani Mara imeonyesha umahiri wake wa kutandaza kabumbu baada ya kuichapa bao 1-0 timu ya Chuo kikuu cha Mwalimu J.K. Nyerere (MJNUAT) katika mechi ya kirafiki iliyofanyika katika viwanja vya mgodi huo.
Mechi hiyo ilikuwa na ushindani mkubwa ambapo kila timu ikitafuta kuibuka na ushindi na mpaka kufikia mapumziko timu zote zilikuwa hazijafungana. Katika kipindi cha pili timu mwenyeji ya North Mara ilifanikiwa kupata bao ambapo timu pinzani haikufanikiwa kusawazisha bao hilo.
Mgodi wa Barrick North mara mbali na kuwa na timu nzuri ya soka unazo timu za wafanyakazi ambazo zimekuwa zikitamba katika michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa netball ,mpira wa kikapu (Basketball) na timu ya riadha ambayo imefanikiwa kushiriki katika riadha mbalimbali za ndani na nje ya nchi.
Pia mgodi imekuwa ukidhamini michezo mbalimbali katika jamii ikiwemo mashindano ya mpira wa miguu kwa vijana – yajulikanayo kwa jina la Mahusiano Cup yanayojumuisha timu za vijana kutoka vijiji vinavyozunguka mgodi ambayo yamekuwa yakifanyika kila mwaka.
Kwa kushiriki katika mashindano haya kila mwaka, vijana wanapata fursa ya kuonesha na kukuza vipaji vyao vya michezo, kujenga afya zao kimwili na kiakili, kufahamiana, kujifunza ushirikiano na nidhamu, kubadilishana mawazo na hata uzoefu kwa upendo.
Aidha, mamia ya wananchi wanaokutanishwa na mashindano ya Mahusiano Cup wanapata pia fursa ya kuelimishwa jinsi mgodi unavyochangia maendeleo yao ya kijamii na kiuchumi.

About the author

mzalendoeditor