Featured Kitaifa

WAZIRI CHANA AMTEUA ALLY MAYAI

Written by mzalendoeditor

DODOMA,

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb), anawajulisha wadau wa michezo na Watanzania wote kuwa Taifa letu limeteuliwa kuwa Mjumbe katika Bodi ya Ushauri wa Michezo ya Jumuiya ya Madola (Commonwealth Advisory Body on Sport – CABOS) kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia 2023-2025. 

Hatua hiyo inatokana na kuimarika kwa nchi yetu katika nyanja za diplomasia ikiwemo ya michezo katika uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. 

Kwa uteuzi huo, Bw. Alli Mayay Tembele ataiwakilisha Tanzania katika Bodi 

ya CABOS na kuwa Mjumbe mwakilishi wa Bara la Afrika. Bw. Alli Mayay kwa sasa ndiye Kaimu Mkurugenzi Maendeleo ya Michezo nchini. Kiuzoefu Bw. Alli Mayay ni mwanamichezo nguli na Nahodha mstaafu wa Timu ya Taifa ya (Taifa Stars) na ni kocha wa mpira wa miguu kitaaluma. 

CABOS ni chombo cha kumshauri Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola na Serikali wanachama kuhakikisha kunakuwepo ushirikishwaji thabiti wa Serikali na uwakilishi katika maendeleo ya sera na utekelezaji wake kwa kuzingatia maadili na matarajio yaliyowekwa ndani ya Mkataba wa Jumuiya hiyo. 

Waziri Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb), anampongeza Bw. Mayay na kumtakia uekelezaji mwema wa majukumu yake. 

Eleuteri Mangi 

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI WIZARA YA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO 

About the author

mzalendoeditor