Featured Kitaifa

RAIS SAMIA APOKEA TAARIFA YA KIKOSI KAZI

Written by mzalendoeditor

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Kikosi Kazi kuhusu Uratibu maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa kutoka kwa Mwenyekiti wa Kikosi Kazi hicho Profesa Rwekaza Mukandala katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Oktoba, 2022. 

………………….

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Sheria ambazo zinahitaji marekebisho madogo zitafanyiwa kazi haraka huku nyingine zitachukua muda kidogo kulingana na muda wa mchakato wa utekelezaji.

Rais Samia amesema hayo leo wakati akipokea Ripoti ya Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa Ikulu jijini Dar es Salaam. 

Aidha, miongoni mwa mapendekezo yaliyotolewa na Kikosi Kazi ni kuruhusiwa kufanyika kwa mikutano ya hadhara kwa mujibu wa Katiba na Sheria pamoja na kuzingatia 40% ya jinsi katika vyombo vya maamuzi vya vyama vya siasa.

Rais Samia ameunga mkono pendekezo la kufanya marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa kwani kutumia Sheria na Kanuni za awali zingeendelea kusababisha changamoto na dosari zilizokuwa zikijitokeza mwanzoni.  

Rais Samia pia amevitaka vyama vya siasa kutathmini mienendo ya vyama vyao hasa kuzingatia usawa wa kijinsia, matumizi mazuri ya fedha, utawala bora na kutokomeza ukatili wa kijinsia kwa kuwawezesha wanawake kugombea nafasi muhimu.  

Vile vile, Kikosi Kazi hicho kimependekeza utaratibu mpya wa kupata Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, utendaji wa Tume uruhusiwe kuhojiwa kwenye Mahakama ya Juu na pia isilazimike kufuata amri ya mtu yeyote, Idara yoyote ya Serikali, Chama chochote cha siasa au Taasisi yoyote.

Kikosi Kazi hicho chenye Wajumbe 24 na kilichowasilisha maeneo 9 ya kufanyiwa kazi, kimependekeza matokeo ya Uchaguzi wa Rais yahojiwe kwenye Mahakama ya Juu mara itakapoanzishwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Kikosi Kazi kuhusu Uratibu maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa kutoka kwa Mwenyekiti wa Kikosi Kazi hicho Profesa Rwekaza Mukandala katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Oktoba, 2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Kikosi Kazi kuhusu Uratibu maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa kutoka kwa Mwenyekiti wa Kikosi Kazi hicho Profesa Rwekaza Mukandala katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Oktoba, 2022.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi mbalimbali pamoja na Wajumbe wa Kikosi Kazi kuhusu Uratibu maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Oktoba, 2022.  Viongozi pamoja na Wajumbe wa Kikosi Kazi kuhusu Uratibu maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa wakisikiliza hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Oktoba, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mwenyekiti wa Kikosi Kazi kuhusu Uratibu maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa Profesa Rwekaza Mukandala, Makamu Mwenyekiti Hamad Rashid Mohamed pamoja na Wajumbe wa Kikosi Kazi hicho mara baada ya kupokea Ripoti yao Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Oktoba, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Mwenyekiti wa Kikosi Kazi kuhusu Uratibu maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa Profesa Rwekaza Mukandala pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Kikosi Kazi hicho Hamad Rashid Mohamed mara baada ya kupokea Ripoti ya Kikosi Kazi hicho Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 21 Oktoba, 2022. PICHA NA IKULU

About the author

mzalendoeditor