Featured Michezo

SIMBA YA KIMATAIFA, YAUNGURUMA NCHINI ANGOLA

Written by mzalendoeditor

Na Odilo Bolgas MZALENDO BLOG 

SIMBA ya Kimataifa Yaunguruma nchini Angola baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3_1 dhidi ya wenyeji  Primiero de Agosto  katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika .

Mabao ya Simba yamefungwa na  Clatous Chama dakika ya 8,beki  Israel Mwenda dakika ya 63 na Moses Phiri dakika ya 76.

Wenyeji walipata bao la kufuatia machozi dakika ya 78 likifungwa kwa mkwaju wa penalti na Dago.

Simba imejiweka katika nafasi nzuri ya kutinga hatua ya Makundi Mechi ya marudiano itapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa Oktoba 16 

About the author

mzalendoeditor