Featured Kitaifa

RAIS SAMIA ATAKA VIONGOZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

Written by mzalendoeditor

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria kuzindua rasmi Soko Kuu la Njombe Mjini mkoani Njombe tarehe 10 Agosti, 2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kama ishara ya kuzindua rasmi Soko Kuu la Njombe Mjini katika hafla iliyofanyika mkoani Njombe tarehe 10 Agosti, 2022.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wafanyabiashara wa matunda na viatu katika Soko Kuu la Njombe mara baada ya kulizindua Soko hilo tarehe 10 Agosti, 2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitembelea Soko Kuu la Njombe Mjini mara baada ya kulizindua rasmi Soko hilo tarehe 10 Agosti, 2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Mkoa wa Njombe mara baada ya kuzindua Soko Kuu la Njombe Mjini tarehe 10 Agosti, 2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mwenyekiti wa Kampuni ya Tanganyika Wattle ltd Jaswant Singh Rai kuhusu utendaji kazi wa kiwanda hicho ikiwemo uzalishaji wa umeme ambao hutumika kiwandani hapo pamoja na kuiuzia Tanesco kwa ajili ya matumizi ya Wananchi tarehe 10 Agosti, 2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitembelea na kukagua kinu cha kufua Umeme katika Kiwanda cha TANWAT Miwati Mkoani Njombe tarehe 10 Agosti, 2022. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Mkoa wa Njombe katika Mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba Mkoani humo tarehe 10 Agosti, 2022.

******************************

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali imezuia kukata na kupandisha hadhi maeneo ya utawala kwa sababu yanaongeza gharama kwa Serikali.

Rais Samia amesema hayo leo wakati akihutubia wananchi wa Njombe katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba.

Aidha, Rais Samia amesema mwelekeo wa Serikali ni kunyanyua hali ya uchumi wa nchi ili kuinua hali ya maisha ya mwananchi mmoja mmoja.  

Rais Samia pia ametoa wito kwa Viongozi nchini kusimamia ipasavyo miradi inayotekelezwa na Serikali ili kuwajengea fursa Watanzania kufanya shughuli za maendeleo na kuinua kipato.

Vile vile, Rais Samia amewataka Viongozi wa Kata, Wilaya na Mikoa kuhudumia wananchi na kutatua kero zao kwa kuzingatia utawala bora.

About the author

mzalendoeditor