Featured Kitaifa

RC MAKALLA ATAKA TAASISI NA WANANCHI KUYALINDA MAENEO NA KUYAENDELEZA ILI YASIVAMIWE 

Written by mzalendoeditor
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amewaonya Wananchi Wenye tabia ya kuvamia maeneo ya Taasisi na watu binafsi na kujenga kuacha tabia hiyo Mara moja kwakuwa ni kosa la jinai kwa mujibu wa sheria.
RC Makalla ametoa maelekezo hayo wakati wa kikao Kilichojumuisha Wakuu wa Wilaya, Kamati za ulinzi na usalama, Wakurugenzi, Wastahiki Meya, makatibu tawala, Wanyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata/ Mitaa ambapo amesema Serikali haitowafumbia macho Wananchi watakaovamia maeneo.
Aidha RC Makalla ameelekeza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuweka Mkazo kwenye usikilizaji na utatuzi wa changamoto ya migogoro ya Ardhi.
Pamoja na hayo RC Makalla amezielekeza Taasisi na Wananchi kuyalinda na kuyaendeleza maeneo yao ili yasivamiwe huku akiwataka Wananchi kuhakikisha wanajiridhisha na Nyaraka na taarifa za Serikali ya mtaa kabla ya kununua eneo.
============
RC MAKALLA: ATANGAZA USAFI BARABARA KUU NA DAR YA KIJANI
– Aelekeza Barabara kuu kusafishwa na kufungwa mifumo ya umwagiliaji.
– Asisitiza Upandaji miti na bustani za watu kupumzika.
– Viongozi wa Machinga wajitolea kuisaidia Serikali kuwapanga vizuri Machinga Wanaofanya biashara kwenye maeneo yaliyokatazwa.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Amos Makalla ametangaza Operesheni kabambe ya Usafi wa Barabara kuu za Mkoa huo ifikapo Jumamos ya Julai 30 ambapo ameelekeza Wananchi na Wakandarasi wa Kampuni za uzoaji wa taka kushiriki kwenye zoezi Hilo.
RC Makalla amesema hayo wakati wa kikao kazi maelekezo kilichojumuisha Viongozi kuanzia ngazi ya Wilaya, Kata, Mitaa na Wadau mbalimbali wa maendeleo ambapo amesema Jiji la Dar es salaam Lina uwezo wa kutoka kwenye nafasi ya sita kwa Usafi Barani Africa na kushika nafasi za juu.
Ilikufanikisha zoezi Hilo, RC Makalla ameelekeza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuhitisha kikao na Watendaji wa Kata na Mitaa kabla ya Julai 30 ili kuweka mipango!kazi wa kufanikisha.
Aidha RC Makalla ameelekeza pia Usafi wa Mito na maboresho ya Fukwe huku akiwataka Wakandarasi wa uzoaji wa taka kuhakikisha taka zinazokusanywa zinaondolewa kwa wakati.
Maelekezo ya RC Makalla yamepokelewa kwa mikono miwili na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Wastahiki Meya, Wenyeviti na Watendaji wa Kata/ Mitaa, Wakandarasi wa taka na Wadau mbalimbali wa maendeleo ambapo wameahidi kuyatekeleza kwa ufanisi mkubwa.
Miongoni mwa Barabara kubwa ambazo RC Makalla ameelekeza kufanyiwa Usafi wa Hali ya juu ni Nyerere road, Bagamoyo road, Morogoro road, Mandela Road, Kilwa road, Pugu Road na nyinginezo kwakuwa zinabeba taswira ya Jiji Hilo.

About the author

mzalendoeditor