Featured Kitaifa

MATUKIO KATIKA PICHA WAZIRI MKUU:ASHIRIKI IBADA YA KUMSIMIKA ASKOFU WOLFGANG JOHN PISA WA JIMBO KATOLIKI LINDI

Written by mzalendoeditor

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpongeza Askofu Wolfgang  John Pisa baada ya  askofu huyo kusimikwa  kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi katika ibada iiyofanyika kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi, 

 Askofu Wolfgang John Pisa  akiwa amelala kifudifudi  katika Ibada ya kusimikwa kwake kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Lindi iliyofanyika kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi, Juni 26, 2022. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alishiriki katika Ibada hiyo.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na baadhi ya viongozi walioshiriki katika Ibada ya kumsimika  Askofu wa Jimbo  Katoliki la Lindi  Wolfgang John Pisa wakifuatilia ibada hiyo iliyofanyika kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi, Juni 26, 2022.  Kushoto ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack.

Baadhi ya washiriki wa Ibada ya kusimikwa Askofu Wolfgang John Pisa kuwa Askofu wa Jimbo  Katoliki la Lindi wakifauatilia Ibada hiyo kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi, 

Baadhi ya Mapadri walioshiriki katika Ibada ya kusimikwa Askofu Wolfgang John Pisa kuwa Askofu wa Jimbo  Katoliki la Lindi wakifauatilia Ibada hiyo kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi

(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

About the author

mzalendoeditor