Featured Kitaifa

RAIS SAMIA AZINDUA KITABU CHA SUGU “MUZIKI NA MAISHA

Written by mzalendoeditor

       

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe Samia Suluhu Hassan leo Mei 31, 2022 amezindua kitabu cha mwanamuziki nguli wa Hip Hop, Mr 2 Proud au maarufu kama Sugu kiitwacho muziki na maisha kwenye tamasha la kutimiza miaka 30 katika tasnia hiyo.

Katika tamasha hilo lililoitwa The dream concert, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe Mohamed Mchengerwa, Katibu Mkuu. Dkt, Hassan Abbasi, Naibu Katibu Mkuu, Saidi Yakubu, watendaji wa Wizara na wadau mbalimbali wamehudhuria.

Tamasha hili limepambwa na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali ikiwa ni pamoja na Sugu mwenyewe ambaye ametumbuiza na kukonga nyoyo za mamia ya watu waliohudhuria.

Mhe. Rais amemtunukia tuzo, Sugu huku akimpongeza kuwa miongoni wasanii wenye nyimbo zenye maadili.

About the author

mzalendoeditor