Featured Kitaifa Uncategorized

UTEUZI:RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

Written by mzalendoeditor

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, amemteua Bwana Hassan Omani Kitenge kuwa Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

Kabla ya uteuzi huo Kitenge alikuwa Mkurugenzi wa Mikataba ya Utendaji Kazi Serikalini, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Uteuzi huu umeanza tarehe 01 Mei, 2022.

About the author

mzalendoeditor