Featured Michezo

SIMBA WAREJEA, HASIRA ZOTE KWA MTANI YANGA JUMAMOSI

Written by mzalendoeditor

KIKOSI cha Simba kimerejea Dar es Salaam  baada ya kutolewa na wenyeji, Orlando Pirates katika Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa penalti 4-3 Jijini Johannesburg, Afrika Kusini kufuatia sare ya jumla ya 1-1, kila timu ikishinda 1-0 nyumbani.
Moja kwa moja Simba inaingia kambini kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya mahasimu, Yanga Jumamosi Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

About the author

mzalendoeditor