Mwanamke mmoja wa Afrika Kusini ambaye alifanya matumizi makubwa baada ya kupokea kimakosa karibu dola milioni 1 (£700,000) katika akaunti yake ya benki amefungwa miaka mitano jela.
Sibongile Mani alipokea randi milioni 14 badala ya randi 1,400 pekee alizostahili kupata 2017 na kuanza kuzitumia mara moja.
Pesa hizo zilitoka zilikuwa ni za Mpango wa Kitaifa wa Msaada wa Kifedha kwa Wanafunzi (NSFAS) kupitia kampuni ya huduma za malipo, Intellimali, alipokuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Walter Sisulu. Lakini hakuripoti kosa hilo.
Badala yake, alianza kutumia pesa hizo ndani ya masaa mawili baada ya kuzipokea
CHANZO:BBCSWAHILI