Uncategorized

KAMATI YA PAC YAKAGUA MRADI WA MABORESHO YA BANDARI YA TANGA

Written by mzalendoeditor

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wakisikiliza maelezo ya jinsi ‘Flow meter’ inavyofanya kazi kutoka kwa opareta wa kipimo hicho Benjamini Kisaki, wajumbe hao wametembelea na kukagua mradi wa maboresho ya Bandari ya Tanga.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Mheshimiwa Naghenjwa Kaboyoka akizungumza na watendaji wa Mamlaka ya Bandari wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa maboresho ya Bandari ya Tanga.

Mkurugenzi wa Uhandisi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Baraka Mdima alikiwaeleza wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) maboresho mbalimbali yanayofanyika katika Bandari ya Tanga wakati wajumbe hao walipotembelea na kukagua mradi huo.

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wakikagua mradi wa maboresho ya Bandari ya Tanga 

PICHA NA OFISI YA BUNGE

About the author

mzalendoeditor