WAZIRI wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda wa Zanzibar, Omar Said Shaaban atakuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika baina ya wenyeji, Simba SC dhidi ya RSB Berkane ya Morocco.

Mchezo huo wa Kundi D utafanyika Jumapili Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam kuanzia Saa 10:00 jioni.
Mechi ya kwanza wiki iliyopita Berkane ilishinda 2-0 mjini Berkane na sasa ndio inaongoza Kundi hilo kwa pointi zake sita, ikifuatiwa na Simba na US Gendamarie ya Niger zenye pointi nne kila moja, wakati ASEC ya Ivory Cost yenye pointi tatu inashika mkia baada ya mechi tatu za awali.
Previous articleTANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO KUKABILIANA NA UJANGILI BARANI AFRIKA
Next articleRAIS SAMIA ATETA NA KIKOSI KAZI CHA URATIBU MAONI YA WADAU WA DEMOKRASIA YA VYAMA VINGI VYA SIASA IKULU CHAMWINO DODOMA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here