Featured Kitaifa

SERIKALI KUONGEZA NGUVU MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

Written by mzalendoeditor

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera,Bunge na Uratibu William Lukuvi,akizungumza wakati  akizindua Bodi Mpya ya Mfuko wa udhamini wa kudhibiti UKIMWI (AIDS Trust Fund-ATE) hafla iliyofanyika leo Juni 26,2025 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Waziri  wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera,Bunge na Uratibu William Lukuvi (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa Bodi Mpya ya Mfuko wa udhamini wa kudhibiti UKIMWI (AIDS Trust Fund-ATE) hafla iliyofanyika leo Juni 26,2025 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Waziri  wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera,Bunge na Uratibu William Lukuvi (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa Bodi Mpya ya Mfuko wa udhamini wa kudhibiti UKIMWI (AIDS Trust Fund-ATE) hafla iliyofanyika leo Juni 26,2025 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Waziri  wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera,Bunge na Uratibu William Lukuvi (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa Bodi Mpya ya Mfuko wa udhamini wa kudhibiti UKIMWI (AIDS Trust Fund-ATE) hafla iliyofanyika leo Juni 26,2025 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu-Sera,Bunge na Uratibu William Lukuvi,amesema   Serikali imeendelea kuongeza nguvu kubwa katika juhudi mbalimbali za kutokomeza maambukizi ya VVU na UKIMWI nchini.

Mhe.Lukuvi ameyasema hayo leo Juni 26,2025 jijini Dodoma wakati akizindua Bodi Mpya ya Mfuko wa udhamini wa kudhibiti UKIMWI (AIDS Trust Fund-ATE).

Amesema kuwa Serikali imeendelea kuimarisha huduma za kinga,tiba na matunzo pamoja na kuendeleza ushirikiano wa ndani na nje ya nchi katika kuboresha mifumo ya afya.

“Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan ameonyesha dhamira ya kweli katika kuondoa kabisa maambukizi mapya ya VVU kwa kuwekeza  kwenye huduma bora za afya na kuhimiza ushirikiano wa wadau”amesema Mhe.Lukuvi

Aidha Waziri Lukuvi ameitaka Bodi hiyo Mpya kuhakikisha inabuni vyanzo vya kimkakati vya fedha za utekelezaji wa afua za mapambano ugonjwa wa UKIMWI kutokana na upungufu wa asilimia 40 wa fedha za wahisani.

“Bodi hii inapaswa kuimarisha mifumo ya uraghibishi na mawasiliano kwa wananchi ili kuunga mkono mchango wa mfuko huo ikiwa ni pamoja kufanya kampeni za kitaifa za uhamasishaji wa kuchangia mfuko huo.”amesema 
Hata hivyo amefafanua  kuwa bodi hiyo pamoja na kukusanya fedha itakuwa washauri wa sera, wasimamizi wa maadili ya matumizi ya rasilimali na mabalozi wa kutafuta vyanzo vipya vya rasilimali za ndani.
“Hili litajumuisha ushiriki wa sekta binafsi, diaspora, taasisi za kifedha, wabia wa maendeleo na hata kuangalia vyanzo bunifu vya mapato ya kimkakati,”amesema 

Kwa upande wake Mwnyekiti wa Bodi ya ATE ,Sabasaba Moshingi,amesema kuwa bodi hiyo itafanya kazi kwa weledi na ubunifu ili kuongeza vyanzo vya mapato.

“Mhe.Waziri tunakuhakikishia kuwa tutajitahidi kadri ya uwezo na weledi kuisimamia na kuiongoza bodi ya mfuko wa ATF katika kutekeleza majukumu iliyokasimiwa.”amesema Moshingi
Awali, Kaimu Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), Dk.Catherine Joackim, amesema  bodi hiyo itafanya kazi kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2025 hadi 2028.
Dkt.Catherine amesema  kuwa wafadhili wakubwa wa afua za Virusi vya Ukimwi (VVU) na UKIMWI ni pamoja na Mfuko wa Dunia wa Kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund) na serikali ya Marekani kupitia Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na UKIMWI (PEPFAR), Shirika la Misaada la Marekani (USAID) na Idara ya Ulinzi ya Marekani (DoD).
“Serikali ya Marekani huchangia zaidi ya asilimia 35 ya fedha za ,fuko wa Dunia wa Kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund).”amesema Dkt.Catherine

About the author

mzalendoeditor