Featured Kitaifa

MAJENGO YA KUTOLEA HUDUMA ZA DHARURA YAONGEZEKA NCHINI

Written by mzalendoeditor

 

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama, akizungumza wakati akifunga maadhimisho ya wiki ya afya kitaifa pamoja na kuzindua mfuko maalum wa ufadhili wa masomo kwa Madaktari Bingwa na Bobezi Leo Aprili 8,2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama, akizungumza wakati akifunga maadhimisho ya wiki ya afya kitaifa pamoja na kuzindua mfuko maalum wa ufadhili wa masomo kwa Madaktari Bingwa na Bobezi Leo Aprili 8,2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Afya,Dk Godwin Molel,akizungumza wakati wa Kilele Cha Wiki ya Afya  kitaifa  Leo Aprili 8,2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Dk Seif Shekilaghe,akizungumza wakati wa maadhimisho ya wiki ya afya kitaifa pamoja na kuzindua mfuko maalum wa ufadhili wa masomo kwa Madaktari Bingwa na Bobezi Leo Aprili 8,2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama,(hayupo Pichani) wakati akifunga maadhimisho ya wiki ya afya kitaifa pamoja na kuzindua mfuko maalum wa ufadhili wa masomo kwa Madaktari Bingwa na Bobezi Leo Aprili 8,2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

NA.Alex Sonna_DODOMA

SERIKALI  imendelea kuboresha huduma za afya kwa kuongeza idadi ya hospitali zenye majengo ya kutolea huduma za dharura (EMD) kutoka 7 hadi kufikia 116 ndani ya miaka minne ikiwa ni ongezeko la Hospitali 109.

 

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amesema hayo leo Aprili 8, 2025 wakati akifunga maadhimisho ya wiki ya afya kitaifa pamoja na kuzindua mfuko maalum wa ufadhili wa masomo kwa Madaktari Bingwa na Bobezi kwenye ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma.

Waziri Mhagama amesema kukamilika kwa ujenzi wa majengo ya kutolea huduma za dharura kunapunguza vifo na kuokoa maisha kwa wagonjwa wa dharura na wa ajali.

Kuhusu huduma ya magari ya wagonjwa Waziri Mhagama amesema idadi ya magari ya imeongezeka kutoka 540 mwaka 2020 hadi 1,267 jambo linalorahisisha huduma za dharurana kuwafikia wananchi wenye changamoto za afya.

“Magari haya yanakwenda kusaidia kusafirisha watu wenye changamoto za afya wakiwemo akinamama wenye changamoto za uzazi kwa haraka na kuwafikisha katika huduma za rufaa na hivyo kupunguza adha kwa wananchi na kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika,” amesema Mhe. Mhagama.

Aidha, Waziri Mhagama amezishukuru Sekta binafsi nchini kwa kuunga mkono Serikali katika kutoa huduma bora kwa wananchi kuanzia ngazi ya msingi hadi ya Kitaifa.

Kwa upande wake,Naibu Waziri wa Afya,Dk Godwin Molel amesema maendeleo katika sekta ya afya hayajaja kwa bahati mbaya bali ni uchapakazi wa Serikali na Rais Samia Suluhu Hassan.
Akiuzungumzia uwezo wa Waziri wa Afya,Jenista Mhagama amesema anajua kazi yake na amekuwa msaada mkubwa kwao katika utendaji kazi.
Amesema Rais Samia ameweka zaidi ya Sh trilioni 7 katika sekta ya afya ambapo kwa Sasa kazi zinaendelea na kumekuwa na mafanikio makubwa.
Naye,Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,(TAMISEMI) Dk Festo Dugange  akizungumza kwa niaba ya Waziri wa TAMISEMI,Mohammed Mchengerwa amesema maadhimisho hayo yanaumuhimu mkubwa wa kukumbushana katika sekta ya afya pamoja na kuweka mikakati ya pamoja katika sekta hiyo.
Amesema  wameendelea kuboresha sekta hiyo  ili kuhakikisha mwananchi anapata huduma zote muhimu huku akimshukuru Rais Samia kwa maono yake katika sekta hiyo.
Amesema huduma zinaendelea kuimarika kwa kuboresha katika vifaa tiba ambapo katika kipindi cha miaka minne kwa ngazi ya afya ya  msingi zaidi ya Sh  trilioni 1 zimetumiika.
“Kwa dhati kabisa nawapongeza watumishi wa sekta ya afya,tunapoongelea mafanikio huwezi kuwagusa watumishi na viongozi wa sekta ya afya,tuna Kila sababu ya kuwapongeza kwa kazi nzuri,hongereni Sana,”amesema Naibu Waziri Dugange.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Rosemary Senyamule  amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuitendea haki kwa mambo mengi ikiwemo kujenga majengo ngazi ya Zahanati mpaka Hospitali za Kanda.
Mhe.Senyamule amesema wamefanya Mapinduzi makubwa kwa Mkoa wa Dodoma ikiwa ni pamoja na kuongeza vifaa ikiwemo X-ray na hivyo wameboresha huduma za afya.
Amesema mwaka  2010 walikuwa na X ray mashine  10 lakini sasa hivi zipo 30 hivyo Serikali  wanawapunguzia wananchi mwendo wa kutembea umbali mrefu kufuata huduma hiyo.
Awali Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Dk Seif Shekilaghe amesema lengo la kuadhimisha siku hiyo ni kujadiliana uzoefu kwa kushirikiana na wadau kwa kuonesha mafanikio na changamoto.
Amesema kumekuwa na malengo maalumu kwa kutoa takwimu wamefikia wapi katika mambo mbalimbali.
Amesema Serikali imeona ni vyema ifanye kwa wiki nzima na iliambatana kwa kuonesha huduma mbalimbali.
Amesema kupitia kauli mbiu wameonesha walipotoka na walipo lakini miaka ya nyuma ilikuwa huwezi kupata CT Scan hili halikuwepo.
“Tumetoa fursa wananchi kupima na kujua afya zao…tunaimani wananchi watazingatia ushauri na kuweza kujikinga na magonjwa mbalimbali,”amesema Dk Shekilaghe.

About the author

mzalendoeditor