Featured Kitaifa

UCSAF YAJIVUNIA MAFANIKIO YAKE KIPINDI CHA MIAKA MINNE YA UONGOZI WA RAIS SAMIA

Written by mzalendoeditor

 

Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Mhandisi Peter Mwasalyanda,akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio na mwelekeo wa taasisi hiyo  katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita leo Machi 27, 2025, katika Ofisi za Idara ya Habari – MAELEZO, jijini Dodoma

 

Sehemu ya Waandishi wa habari wakimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Mhandisi Peter Mwasalyanda,(hayupo pichani) wakati akiwasilisha mafanikio na mwelekeo wa taasisi hiyo  katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita leo Machi 27, 2025, katika Ofisi za Idara ya Habari – MAELEZO, jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna_DODOMA
KATIKA kipindi cha Miaka minne ya Serikali ya awamu sita,Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) umesema jumla ya walimu wapatao 1585 wamepatiwa mafunzo juu umuhimu wa matumizi ya TEHAMA.
Hayo yameelezwa leo Machi 27,2025 na Mtendaji Mkuu wa UCSAF Mhandisi Peter Mwasalyanda,wakati  akitoa taarifa ya mafanikio na Mwelekeo wa Taasisi hiyo katika kipindi cha miaka 4 ya uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika Ofisi za Idara ya Habari-MAELEZO Jijini Dodoma.
Mhandisi Mwasalyanda amesema kuwa kitendo cha kuwapatia elimu ya TEHAMA walimu hao ni hatua kubwa ya kuwawezeshe kutenda kazi zao kwa kujiamini na kwa uzoefu na kazi zao.
Ameeleza kuwa elimu hiyo kwa walimu itawawezesha pia kuvielewa vifaa vya tehama hata pale vinaposumbua wasipate usumbufu wa kuwatafuta mafundi kwa mambo ambayo wanaweza kuyafanya wenyewe na kuwafundisha wanafunzi kwa uelewa zaidi.
Aidha amesema kuwa kutokana na umuhimu wa elimu ya TEHAMA,UCSAF imepeleka vifaa katika shule zenye uhitaji maalumu vyenye gharama ya shilingi bilioni 1.8.
Akizungumzia kuhusu uboreshaji wa mawasiliano amesema kuwa jumla ya minara 758 imejengwa na inatarajiwa kufikia Mei 12 mwaka huu itakuwa imekamilika.
Aidha Mhandisi Peter amesema kupitia Mradi huo vijiji 1407,Kata 713,wilaya 127 katika mikoa 26 zitanufaika na mpaka sasa minara 430 Sawa na asilimia 57 imeshajengwa kati ya 758.

“Pamoja na mradi huo pia tumeboresha minara 304 kuiongezea nguvu kutoka kwenye 2G hadi 3G kwa gharama ya zaidi ya bilioni 5,”

Na kuongeza kuwa “Dhamira ya serikali ni kuona wanachi hawapati changamoto ya Mawasiliano kwani bila Mawasiliano mazuri hata suala la ukuaji wa uchumi utakuwa mdogo kwani biashara nyingi kwa sasa zinategemea mtandao madhubuti hivyo jitihada hizi za kuboresha Mawasiliano nchini zinalenga kuchochea maendeleo, “amesema Mhandisi Mwasalyanda

Mhandisi Mwasalyanda amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri  inatambua umuhimu wa shirika la Posta nchini na hivyo katika kipindi cha miaka minne Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote imekuwa ikiliwezesha shirika la Posta kwa kulipatia vifaa vya TEHAMA ili shirika liweze kutoa huduma kidigitali.

Ambapo tarehe 12 Julai 2024, UCSAF ilinunua PDA 250 na kuwakabidhi Shirika la Posta. Gharama za utekelezaji wa mradi huu ni kiasi cha TZS 161,926,471/=.

Mwezi Aprili 2025, UCSAF itakabidhi vifaa vingine 250 kwa shirika la Posta vyenye thamani ya TZS 161,926,471/=

About the author

mzalendoeditor