Featured Kitaifa

WAZIRI MASAUNI ATETA NA KAMISHNA MKUU WA UNHCR, FILIPPO GRANDI, JIJINI GENEVA NCHINI USWISI

Written by mzalendoeditor

 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akizungumza na Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Filippo Grandi, Ukumbi wa Mikutano wa Umoja wa Mataifa katika Kikao cha 73 cha Kamati Tendaji ya Shirika hilo jijini Geneva, nchini Uswisi

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (Wapili kulia) akimsikiliza Msaidizi wa Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Gillian Triggs, akizungumzia masuala ya Wakimbizi, katika ukumbi mdogo wa Mikutano wa Umoja wa Mataifa wakati wa Kikao cha 73 cha Kamati Tendaji ya Shirika hilo jijini Geneva, nchini Uswisi, leo. Kulia ni Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania, nchini Uswisi, Maimuna Tarishi na watatu kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Sudi Mwakibasi. 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (Wapili kulia) akizungumza na Msaidizi wa Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Gillian Triggs, kuhusu masuala ya Wakimbizi katika ukumbi mdogo wa Mikutano wa Umoja wa Mataifa wakati wa Kikao cha 73 cha Kamati Tendaji ya Shirika hilo jijini Geneva, nchini Uswisi, leo. Wapili kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Sudi Mwakibasi. 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akifurahi jambo na Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania, nchini Uswisi, Maimuna Tarishi (katikati) na Mkurugenzi wa Idara ya Huduma kwa Wakimbizi, Sudi Mwakibasi, wakati alipokuwa anatoka kuzungumza na Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Filippo Grandi katika Kikao cha 73 cha Kamati Tendaji ya Shirika hilo jijini Geneva, nchini Uswisi, leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

About the author

mzalendoeditor