Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray akizungumza na Viongozi Chipukizi wakati wa uzinduzi wa Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Wengine ni wageni waalikwa.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wakwanza kulia) akimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo (hayupo pichani) wakati akitoa maelezo ya awali kuhusu taasisi hiyo kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri huyo kuzindua rasmi Programu ya Mafunzo kwa Viongozi Chipukizi Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifurahia jambo wakati Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) alipokuwa akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (wapili kutoka kulia) akiwa katika uzinduzi wa Programu ya Mafunzo kwa Viongozi Chipukizi Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo. Wengine ni Watendaji wa taasisi hiyo.



Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (katikati waliokaaa) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi Chipukizi mara baada ya Naibu Waziri huyo kuzindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya Viongozi Chipukizi wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (hayupo pichani) wakati akizindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi hao Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Wengine ni wageni waalikwa.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Taasisi ya UONGOZI mara baada ya kuzindua Programu ya Mafunzo kwa Viongozi Chipukizi Awamu ya Kwanza yaliofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo.
Na Veonica Mwafisi-Dar es Salaam
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Regina Qwaray ametoa wito kwa Viongozi kuendelea kujifunza siku kwa siku ili kuendana na mabadiliko ya kiteknolojia na kitamaduni yatakayowezesha kubuni mikakati mbalimbali ya kuboresha utendaji kwa ustawi wa taifa.
Mhe. Qwaray ameyasema hayo leo tarehe 11 Disemba, 2025 jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na Viongozi Chipukizi kabla ya kuzindua Programu ya Viongozi hao.
Amesema ili mtu aweze kuwa kiongozi mzuri, ni lazima aendelee kujifunza kila siku kwa lengo la kuweza kukabiliana na changamoto za kiuongozi ikiwemo kubuni mbinu mbalimbali za kusimamia mabadiliko ya kimfumo, kiutawala, kiuchumi, kiteknolojia na kitamaduni yanayojitokeza kila siku.
Mhe. Qwaray amewashukuru na kuwapongeza washirika kutoka Finland na HAUS kwa kukubali kushirikiana na Taasisi ya UONGOZI kubuni na kuandaa programu hii maalumu kwa viongozi na taifa kwa ujumla kwani ina umuhimu wa pekee katika kuendeleza viongozi nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla.
Aidha, amewasisitiza Viongozi kushirikiana na watumishi walio chini yao kwa kuwaelekeza kazi badala ya kuwaacha na kuwaona ni tatizo katika utekelezaji wa majukumu yao.
Kiongozi usiwe mchoyo kufundisha walio chini yako, tuwafundishe, tunakua, tutengeneze viongozi wa baadae, tusishikilie madaraka, tutengeneze viongozi wengi kadri tuwezavyo, Kiongozi hutakiwi kushikilia kila kitu, shirikisha wenzio ili upate mawazo mapya, kuboresha utendaji na kufikia malengo mahususi yaliyowekwa kwa ustawi wa taifa, Mhe. Qwaray amesisitiza.
Amesema Tanzania inaendelea kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs 2030), Ajenda ya Maendeleo ya Afrika (Agenda 2063) na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na malengo hayo yameweka bayana kuwa mabadiliko ya kiuongozi ni muhimu kwani ndiyo nguzo kuu ya kufikia malengo yaliyowekwa huku akitolea mfano Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kuwa imeweka malengo ya kuwa na uchumi wa dola trilioni moja ifikapo mwaka 2050.
“Ni dhahiri hatuwezi kufikia lengo hili kama tusipojipanga na kuweka mikakati madhubuti ya kutuwezesha kufikia malengo yetu.”
Ametaja moja ya mikakati hiyo ni pamoja na kuwa na nguvu kazi yenye uwezo na motisha pamoja na kuwajengea uwezo viongozi kupitia mafunzo kama haya.
Programu hii ni muhimu sana kwani itasaidia Serikali kuwa na viongozi watakaotimiza matarajio ya wananchi.
“Nina imani kuwa maarifa na ujuzi utakaotolewa kwa washiriki wa programu hii utawapa msingi bora na utayari kuongoza na kutoa huduma bora kwa wanachi.
Mhe. Qwaray amewashauri viongozi kujifanyia tathmini ili kutambua uwezo na udhaifu wao kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kuboresha utendaji hasa kwenye eneo la mapungufu.
Akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri kuzindua Programu hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo amesema Taasisi yao imekuwa ikitoa mafunzo mbalimbali ya uongozi ili kuwa na viongozi bora katika taifa.
“Kunaweza kukawa na mifumo mizuri lakini viongozi sio wazuri, hivyo mafunzo tunayoyatoa yanasaidia kuwajenga viongozi kuendana na mifumo mizuri iliyopo, Bw. Kadari ameongeza.