Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 10,2026 jijini Dodoma kuhusu Bajeti ya Serikali ya mwaka 2026/27 inayotarajiwa kusomwa kesho Juni 11,2026 bungeni Dodoma.
Na.Alex Sonna,Mzalendo blog-DODOMA
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, amesema Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/27 ni ya kihistoria na ya kipekee kwa kuwa ndiyo ya kwanza kutekeleza kwa vitendo Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2026/27–2030/31) pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 10,2026 jijini Dodoma katika mkutano wa kuelezea dondoo za bajeti kabla ya kuwasilishwa rasmi bungeni Juni 11, 2026, Waziri Omar amesema bajeti hiyo imejikita katika kuimarisha ukuaji wa uchumi, kuongeza fursa za ajira, kuharakisha utekelezaji wa miradi ya kimkakati na kuboresha ustawi wa wananchi.
Amesema Serikali inatarajia kutumia jumla ya Shilingi trilioni 62.3 katika mwaka wa fedha 2026/27, ambapo sehemu kubwa ya fedha hizo itaelekezwa kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma muhimu za kijamii.
“Bajeti hii inakuja katika kipindi muhimu ambapo Taifa limeanza safari ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Dhamira yetu ni kuhakikisha ukuaji wa uchumi unakuwa jumuishi, endelevu na wenye manufaa kwa wananchi wote,” amesema Waziri Omar.
Ametaja baadhi ya maeneo yatakayopatiwa kipaumbele kuwa ni ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), uboreshaji wa miundombinu ya barabara, upanuzi wa huduma za maji na nishati, pamoja na uwekezaji katika maendeleo ya rasilimali watu kupitia elimu, afya na ukuzaji wa ujuzi.
Kwa upande wa mapato, Waziri Omar amesema Serikali inalenga kukusanya Shilingi trilioni 46.8 kutoka vyanzo vya ndani, hatua inayodhihirisha kuongezeka kwa uwezo wa Taifa kujitegemea katika kugharamia shughuli zake za maendeleo.
Aidha, ameeleza kuwa utekelezaji wa Bajeti ya mwaka 2025/26 umeendelea kuonyesha mafanikio makubwa kutokana na mwenendo mzuri wa ukusanyaji wa mapato ya ndani, hali iliyowezesha Serikali kufikia malengo mengi yaliyowekwa katika kipindi hicho.
Akizungumzia maboresho ya kodi, ada na tozo mbalimbali, Waziri huyo amesema Serikali ilipokea mapendekezo 727 kutoka kwa wadau mbalimbali, wakiwemo wafanyabiashara, taasisi za umma, sekta binafsi, mashirika yasiyo ya kiserikali, taasisi za elimu na wananchi binafsi.
Aidha amefafanua kuwa kati ya mapendekezo hayo, 125 yalikubaliwa moja kwa moja, 121 yakafanyiwa maboresho kabla ya kupitishwa, huku mengine yakielekezwa kwa taasisi husika kwa uchambuzi zaidi au kutokubaliwa kutokana na sababu za kiuchumi, kisera na kiutawala.
“Lengo la maboresho haya ni kukuza uchumi, kuvutia uwekezaji, kuongeza wigo wa walipa kodi, kuondoa baadhi ya kero za kikodi na kuifanya mifumo ya kodi kuwa rafiki zaidi kwa walipa kodi,” amesema
Waziri Omar amebainisha kuwa mchakato wa kuandaa mapendekezo ya maboresho ya kodi ulihusisha ushiriki mpana wa wadau kupitia Kamati ya Wataalam ya Maboresho ya Kodi (Taskforce on Tax Reforms) pamoja na Kamati ya Ushauri ya Ngazi ya Juu ya Think Tank, hatua iliyowezesha kupatikana kwa maoni ya kitaalamu yanayozingatia maslahi mapana ya Taifa.
Waziri Omar amewataka Watanzania kuendelea kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi kwa hiari na kwa wakati, huku Serikali ikiendelea kuimarisha usimamizi na matumizi ya fedha za umma ili kuhakikisha zinatumika kwa ufanisi na kuleta matokeo chanya kwa maendeleo ya wananchi.
Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi kufuatilia kwa karibu hotuba ya Bajeti ya Serikali ya mwaka 2026/27 itakayowasilishwa bungeni Juni 11, 2026, ili kupata ufahamu wa kina kuhusu vipaumbele, mikakati na mwelekeo wa maendeleo ya Taifa katika mwaka mpya wa fedhaNa.Alex Sonna,Mzalendo blog-DODOMA
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, amesema Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/27 ni ya kihistoria na ya kipekee kwa kuwa ndiyo ya kwanza kutekeleza kwa vitendo Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2026/27–2030/31) pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 10,2026 jijini Dodoma katika mkutano wa kuelezea dondoo za bajeti kabla ya kuwasilishwa rasmi bungeni Juni 11, 2026, Waziri Omar amesema bajeti hiyo imejikita katika kuimarisha ukuaji wa uchumi, kuongeza fursa za ajira, kuharakisha utekelezaji wa miradi ya kimkakati na kuboresha ustawi wa wananchi.
Amesema Serikali inatarajia kutumia jumla ya Shilingi trilioni 62.3 katika mwaka wa fedha 2026/27, ambapo sehemu kubwa ya fedha hizo itaelekezwa kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma muhimu za kijamii.
“Bajeti hii inakuja katika kipindi muhimu ambapo Taifa limeanza safari ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Dhamira yetu ni kuhakikisha ukuaji wa uchumi unakuwa jumuishi, endelevu na wenye manufaa kwa wananchi wote,” amesema Waziri Omar.
Ametaja baadhi ya maeneo yatakayopatiwa kipaumbele kuwa ni ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), uboreshaji wa miundombinu ya barabara, upanuzi wa huduma za maji na nishati, pamoja na uwekezaji katika maendeleo ya rasilimali watu kupitia elimu, afya na ukuzaji wa ujuzi.
Kwa upande wa mapato, Waziri Omar amesema Serikali inalenga kukusanya Shilingi trilioni 46.8 kutoka vyanzo vya ndani, hatua inayodhihirisha kuongezeka kwa uwezo wa Taifa kujitegemea katika kugharamia shughuli zake za maendeleo.
Aidha, ameeleza kuwa utekelezaji wa Bajeti ya mwaka 2025/26 umeendelea kuonyesha mafanikio makubwa kutokana na mwenendo mzuri wa ukusanyaji wa mapato ya ndani, hali iliyowezesha Serikali kufikia malengo mengi yaliyowekwa katika kipindi hicho.
Akizungumzia maboresho ya kodi, ada na tozo mbalimbali, Waziri huyo amesema Serikali ilipokea mapendekezo 727 kutoka kwa wadau mbalimbali, wakiwemo wafanyabiashara, taasisi za umma, sekta binafsi, mashirika yasiyo ya kiserikali, taasisi za elimu na wananchi binafsi.
Aidha amefafanua kuwa kati ya mapendekezo hayo, 125 yalikubaliwa moja kwa moja, 121 yakafanyiwa maboresho kabla ya kupitishwa, huku mengine yakielekezwa kwa taasisi husika kwa uchambuzi zaidi au kutokubaliwa kutokana na sababu za kiuchumi, kisera na kiutawala.
“Lengo la maboresho haya ni kukuza uchumi, kuvutia uwekezaji, kuongeza wigo wa walipa kodi, kuondoa baadhi ya kero za kikodi na kuifanya mifumo ya kodi kuwa rafiki zaidi kwa walipa kodi,” amesema
Waziri Omar amebainisha kuwa mchakato wa kuandaa mapendekezo ya maboresho ya kodi ulihusisha ushiriki mpana wa wadau kupitia Kamati ya Wataalam ya Maboresho ya Kodi (Taskforce on Tax Reforms) pamoja na Kamati ya Ushauri ya Ngazi ya Juu ya Think Tank, hatua iliyowezesha kupatikana kwa maoni ya kitaalamu yanayozingatia maslahi mapana ya Taifa.
Waziri Omar amewataka Watanzania kuendelea kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi kwa hiari na kwa wakati, huku Serikali ikiendelea kuimarisha usimamizi na matumizi ya fedha za umma ili kuhakikisha zinatumika kwa ufanisi na kuleta matokeo chanya kwa maendeleo ya wananchi.
Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi kufuatilia kwa karibu hotuba ya Bajeti ya Serikali ya mwaka 2026/27 itakayowasilishwa bungeni Juni 11, 2026, ili kupata ufahamu wa kina kuhusu vipaumbele, mikakati na mwelekeo wa maendeleo ya Taifa katika mwaka mpya wa fedha