Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewahimiza walimu nchini wasichoke kujiendeleza kitaaluma ili kuendana na mabadiliko yanayoendelea kutokea Duniani.
Dkt. Biteko amesema hayo Oktoba 16, 2025 katika Manispaa ya Musoma, mkoani Mara wakati akifungua Semina ya Viongozi wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) kanda ya Ziwa na Ziwa Magharibi iliyoshirikisha viongozi kutoka mikoa minane.