MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Chifu Hangaya, ambaye ni Mkuu wa Machifu nchini, akiwa kwenye Kituo cha Hifadhi ya Utamaduni wa Kabila la Wasukuma – Bujora, Magu, mkoani Mwanza, leo Jumamosi, tarehe 21 Juni 2025
Rais Dkt. Samia Chifu Hangaya, anashiriki Tamasha la Bulabu, linalofanyika katika Uwanja wa Bulabu, Kisea. Pichani, kushoto kwa Mhe. Rais ni Chifu Antonia Tonisizya, Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu, Tanzania na kulia kwake ni Chifu Nyamilonda II, Aron Mikomangwa, ambaye ni Katibu wa Machifu.