Featured Kitaifa

GST YAANIKA MAFANIKIO YAKE MIAKA MINNE YA RAIS SAMIA

Written by mzalendoeditor

KAIMU Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) Bw.Nokta Banteze,akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Mafanikio na Mwelekeo wa taasisi hiyo katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita leo Machi 27,2025,katika Ofisi za Idara ya Habari-MAELEZO,jijini Dodoma.

SEHEMU ya Waandishi wa habari wakimsikiliza Kaimu  Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) Bw.Nokta Banteze (hayupo pichani) wakati akiwasilisha  Mafanikio na Mwelekeo wa taasisi hiyo katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita leo Machi 27,2025,katika Ofisi za Idara ya Habari-MAELEZO,jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

TAASISI   ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) inatarajia kujenga maabara ya kisasa  katika mkoa wa Dodoma kwa ajili kuimarisha uchunguzi wa  sampuli za madini nchini ili kuchochea shughuli za utafiti nchini na hivyo kuhamasisha ukuaji wa Sekta ya Madini.

Hayo yameelezwa leo Machi 27,2025 na Kaimu  Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) Bw.Nokta Banteze,wakati  akitoa taarifa ya mafanikio na Mwelekeo wa Taasisi hiyo katika kipindi cha miaka 4 ya uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika Ofisi za Idara ya Habari-MAELEZO Jijini Dodoma.

“Maabara hiyo  itakuwa na vifaa vya kisasa na itaweza kufanya uchunguzi wa sampuli za madini nyingi zaidi ikiwemo zinazojumuisha madini ya kimkakati na madini muhimu”amesema Bw.Banteze

Aidha amesema kuwa GST inatarajia  kufanya utafiti wa kina wa jiofizikia kwa kutumia ndege ili kuongeza eneo la nchi lililofanyiwa utafiti huo kutoka asilimia 16 ya sasa hadi asilimia 34. 
Bw.Banteze amesema utafiti huo unatarajiwa kufanyika katika eneo lenye ukubwa wa asilimia 18 ya eneo lote la nchi yetu, Lengo la Serikali ni kufika asilimia 50 ifikapo mwaka 2030. 
“Utafiti huo ukikamilika utakuwa na manufaa mengi kwa nchi yetu katika sekta za madini, kilimo, maji, mazingira, mipango miji na sekta ya ujenzi”,amesema 
Hata hivyo amesema Katika kipindi cha miaka minne  chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, GST imeshuhudia mafanikio makubwa ambayo ni pamoja na Kuongezeka kwa Makusanyo ya ndani  kutoka wastani wa shilingi 1,251,428,472.91 mwaka 2021 hadi shilingi 2,394,211,348 mwaka 2023/2024, sawa na ongezeko la asilimia 91.32.
“Kuongezeka kwa idadi ya sampuli zinazochunguzwa kutoka wastani wa sampuli 19,184 mwaka 2021 hadi sampuli 25,793 mwaka 2023/2024 sawa na ongezeko la asilimia 34.45. Ongezeko hili limetokana na maboresho makubwa ya maabara yaliyofanyika hasa katika ununuziwa vifaa na mashine za kisasa za uchunguzi wa sampuli,”Amefafanua Banteze.

Pia amesema GST imeshuhudia mageuzi na maboresho makubwa katika utoaji wa huduma zake na utendaji kazi wake kwa ujumla.

“Mafanikio hayo yametokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali pamoja na utayari wa viongozi wetu kuona GST inaimarika zaidi kwa ukuaji endelevu wa Sekta ya Madini.”amesema 

Hata hivyo amesema kuwa GST  kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekamilisha utafiti na uchoraji wa ramani ya jiolojia ya visiwa vya Zanzibar (Unguja na Pemba).

Ambapo amesema  kuwa visiwa vya Zanzibar havijawai kufanyiwa utafiti huo wa jiolojia..

“Matokeo ya utafiti huo yamebaini uwepo wa miamba ya chokaa yenye ubora wa kutengeneza saruji, Madini tembo, Madini ya silica, strontium, vyanzo vya maji ardhi, maeneo yenye vivutio vya utalii wa jiolojia na maeneo hatarishi kwa majanga ya asili ya jiolojia. “amesema Bw.Banteze

Aidha amesema kuwa uchukuaji wa sampuli za mchanga wa bahari kwa ajili ya kuchunguzi madini tembo  katika Kisiwa cha Unguja na Pemba

About the author

mzalendoeditor