Featured Kitaifa

𝗪𝗔𝗟𝗜𝗠𝗨 𝟲𝟰𝟲 𝗪𝗔𝗣𝗔𝗧𝗜𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗙𝗨𝗡𝗭𝗢 𝗞𝗨𝗪𝗘𝗭𝗘𝗦𝗛𝗔 𝗨𝗧𝗘𝗞𝗘𝗟𝗘𝗭𝗔𝗝𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗣𝗔𝗡𝗚𝗢 𝗪𝗔 𝗦𝗛𝗨𝗟𝗘 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗠𝗔 𝗖𝗛𝗜𝗡𝗜 𝗬𝗔 𝗨𝗙𝗔𝗗𝗛𝗜𝗟𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗥𝗔𝗗𝗜 𝗪𝗔 𝗕𝗢𝗢𝗦𝗧

Written by mzalendoeditor

Walimu 646 wa Shule za Msingi Wanufaika na Mafunzo yanayolenga kuwezesha utekelezaji wa Mpango wa Shule Salama kwa Shule za Awali na Msingi ili kumwezesha mwanafunzi kusoma na kumaliza mzunguko wake wa Elimu.

Mafunzo hayo yanayoendeshwa na Serikali chini ya ufadhili wa Mradi wa Kuimarisha Ufundishaji na Ujifunzaji kwa Shule za Awali na Msingi Tanzania (BOOST).

Walimu hao ni wa shule za Msingi kutoka mikoa sita ambayo ni Dodoma, Iringa, Njombe, Mbeya, Songwe, na Ruvuma.

Mafunzo yameanza Machi, 18, 2025 katika Chuo cha Ualimu Klerruu, mkoani Iringa ambapo mada mbalimbali zimejadiliwa ikiwa ni pamoja na ulinzi na usalama wa mtoto, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia, pamoja na umoja wa wazazi na walimu (UWAWA).

About the author

mzalendoeditor