Featured Kimataifa

WATAALAMU WA NGAZI YA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA WAJENGEWA UWEZO WA UELEWA WA MWONGOZO WA UFUATILIAJI NA TATHMINI

Written by mzalendo

Baadhi ya Wajumbe wakifuatilia mawasilisho wakati wa kikao hicho.

Afisa Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu ) Bw. Charlton Charles Meena akitoa wasilisho wakati wa kikao hicho.

Mkurugenzi wa Idara ya Kitaifa ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Serikali Bi. Sakina Mwinyimkuu Ofisi ya Waziri Mkuu akizungumza wakati wa kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Bunge na Uratibu) Bw. Anderson Mutatembwa (hayupo pichani) ili kufungua kikao kazi cha Kujenga Uelewa wa majukumu na Upimaji wa Utendaji wa Serikali ngazi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, tarehe14 Machi, 2024.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bw. Anderson Mutatembwa akizungumza wakatiufunguzi wa kikao kazi cha Kujenga Uelewa wa majukumu na Upimaji wa Utendaji wa Serikali ngazi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma tarehe 14 Machi, 2024.

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

Na Mwandishi wetu.

Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu imeandaa Mwongozo Jumuishi wa Ufuatiliaji na Tathmini kwa lengo la kutoa maelekezo katika hatua za kufuata kwenye ufuatiliaji wa afua za maendeleo, hatua za kitaalamu za maandalizi ya viashiria vya utendaji wa taasisi, kuanisha utaratibu wa kusimamia takwimu zitokanazo na ufuatiliaji wa shughuli za taasisi na kutoa mwongozo wa maandalizi ya taarifa za ufuatiliaji, tathmini, utekelezaji na utendaji wa Serikali.

Akizungumza wakati wa kufungua kikao kazi cha Kujenga Uelewa wa majukumu na Upimaji wa Utendaji wa Serikali ngazi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Dodoma Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Bw. Anderson Mutatembwa amesema Mwongozo huu umewasilishwa katika ngazi ya Makatibu Wakuu, Wakurugenzi na Wakurugenzi Wasaidizi na Wasaidizi wa U&T ngazi ya Wizara hivyo ni hatua muhimu katika kupata uelewa wa pamoja juu ya mwongozo husika na kutoa maoni kabla ya kusainiwa.

“Nisisitize kuwa, Mwongozo huu umekuja wakati muafaka ambapo shughuli za U&T ndani ya Idara na Vitengo vyenu zinatakiwa kufanyika kwa ubora na viwango vinavyotakiwa ” alisema Mutatembwa

Aidha Mutatembwa ameongeza kuwa Mwongozo unaainisha muundo wa usimamizi na majukumu ya kila taasisi kwa ngazi za Kitaifa, Kisekta na Wizara, Idara zinazojitegemea, Mashirika ya Umma, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa hivyo majukumu hayo yanaainisha kazi zinazotakiwa kutekelezwa ili kukamilisha upimaji wa utendaji wa kila taasisi na kuwezesha upatikanaji wa taarifa za utekelezaji na utendaji wa kila siku au pindi zinapohitajika.

“Nisisitize tena, matumizi ya Mwongozo huu yatawezesha Serikali kufuatilia, kutathmini na kupima utendaji wa taasisi zote katika ngazi za kitaifa na kisekta na kujenga msingi wa uwajibikaji wa taasisi husika kwenye mchango wa maendeleo na utoaji wa huduma kwa wananchi” aliongeza Mutatembwa.

Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Kitaifa ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Serikali Bi. Sakina Mwinyimkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu amesema nivizuri kuwa na Muongozo huu ili kuweza kuwa na utendaji ulimzuri kwenye kazi kwa manufaa ya Serikali.

“Naomba uwepo wenu kikamilifu katika kulitimiza kususdi la kuwepo kwetu hapa leo, maana ukiangalia kwa mwaka wa fedha uliopita na huu shauku kubwa imekuwa kwenye namna ya utendaji wa Serikali kwenye kuratibu na kusimamia utendaji wa Serikali na ninyi wenyewe mmekuwa mashahidi tunaporudi kule kwenye utekelezaji wa kazi zetu unaona namna ambavyo tunavyofanya kazi kwa hiyo matokeo yake tunanyang’anyana rasilimali lakini tutakapo kuwa na uratibu mzuri na utekelezaji mzuri wa sera na programu hizo changamoto tutazitatua.” Alisema Bi. Sakina.

Akifunga kikao kazi hicho Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI anayeshughulikia masuala ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Dkt. Wilson Mahela amewasisitiza watendaji kufanya kazi kwa bidii ili kumsaidi Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwatumikia wananchi kwa kufanya tamthimini zenye uhalisia wa maeneo wanayofanyia kazi kwa lengo na kuinua Mapato ya maeneo yao na Nchi kwa ujumla.

“Unakuta kule kwenye halmashari kwasababu tumesema ni upimaji wa Serikali na vyeo mlivyopewa ni vikubwa sana na si kwamba unasimamia tu utendaji kazi wa halmashauri unakuta maafisa kilimo hawajulikani wanawajibika kwa nani unakuta wananchi wanapata shida kwa hiyo maana yangu ni kwamba ninyi mnamajukumu makubwa ya kwenda kusaidia si masuala ya tu ya bajeti bali na kutatua matatizo ya wananchi na mhakikishe mnaelewa hiyo miongozo yote kwa ufasaha zaidi.” Alisisitiza Mahela.

About the author

mzalendo