Featured Michezo

RAIS DK. MWINYI AZURU KABURI LA MAREHEMU RAIS MSTAAF WA ZANZIBAR IDRISSA ABDULWAKIL

Written by mzalendo

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akifurahia jambo wakati akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud na Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja Mhe Galos Nyimbo, alipowasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja kwa ajili ya kuzungumza na Wazee wa Mkoa wa Kusini Unguja leo 16-12-2023.(Picha na Ikulu)

WAZEE wa Mkoa wa Kusini Unguja wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) wakati wa ziara yake katika Mkoa huo mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kusini na kuhudhuria Dua Maalum ya kuwaombea Viongozi na kuiombea Nchi Amani,  iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Mtegani Makunduchi leo 16-12-2023.(Picha na Ikulu).

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi  akizungumza na Wazee wa Mkoa wa Kusini Unguja katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kusini Makunduchi, wakati wa ziara yake na kuhudhuria Dua Maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwaombea Viongozi Wakuu na kuiombea Nchi Amani, iliyofanyika katika  Msikiti Mkuu wa Ijumaa Mtegani Makunduchi leo 16-12-2023.(Picha na Ikulu).

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Wazee wa Mkoa wa Kusini Unguja katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kusini  Makunduchi akiwa katika ziara yake na kuhudhuria dua Maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwaombea Viongozi na kuiombea Nchi Amani iliyofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Mtegani Makunduchi leo 16-12-2023, na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe.Ayoub Mohammed Mahmoud na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Wilaya ya Kusini Mhe.Galos Nyimbo.(Picha na Ikulu).

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa zawadi maalum ya migomba na Kiongozi wa Wazee wa Mkoa wa Kusini Unguja Mzee Mwita Masemo Makungu (kulia kwa Rais) baada ya kumaliza mazungumzo yake na Wazee wa Mkoa huo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja Makunduchi leo 16-12-2023 na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Viongozi na Familia ya Marehemu Rais Mstaaf wa Zanzibar Idrissa Abdulwakili katika kuitikia dua ya kumuombea marehemu ikisomwa na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali, iliyofanyika katika kaburi la marehemu Kijijini kwao Makunduchi, wakati wa ziara yake katika Mkoa wa Kusini Unguja na kuhudhuria dua maalum ya kuwaombea Viongozi Wakuu na kuiombea Nchi Amani, dua hiyo iliyofanyika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa Mtegani Makunduchi na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria.Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Mhe.Haroun Ali Suleiman na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud na Mkuu wa Wilaya ya Kusini Mhe. Galos Nyimbo.(Picha na Ikulu).

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Viongozi na Familia ya Marehemu Sheikh Hassan Bin Ameir, alipofika katika kaburi la marehemu katika Kijiji cha Mtegani Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja, kwa ajili ya kumombea dua  ,akiwa katika ziara yake na kuhudhuria  dua maalum ya kuwaombea Viongozi Wakuu wa Nchi na kuiombea Nchi Amani,iliyofanyika katika msikiti Mkuu wa Ijuma Mtegani Makunduchi leo 16-12-2023.(Picha na Ikulu)

About the author

mzalendo