Featured Kitaifa

WAZIRI JAFO ASHIRIKI ZOEZI LA KUFANYA USAFI NA KUPANDA MITI SHULE YA SEKONDARI KIWANJA CHA NDEGE DODOMA

Written by mzalendoeditor

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt.Selemani Jafo akiongoza zoezi la kufanya usafi lililoenda sambamba na kupanda miti katika shule ya Sekondari Kiwanja cha Ndege ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya siku mazingira Duniani itakayofanyika Juni 5, mwaka huu leo Juni 1,2023 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

IMEELEZWA athari za kimazingira nchini zimechangia  kupanda kwa bei ya vyakula ikiwemo unga wa mahindi kutoka na kukosekana kwa mvua na hata maeneo ilikonyesha ilikuwa ni chini ya wastani.

Hayo yameelezwa leo Juni 1,2023 jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt.Selemani Jafo,wakati akishiriki zoezi la kupanda miti katika shule ya Sekondari Kiwanja cha Ndege ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya siku mazingira Duniani itakayofanyika Juni 5, mwaka huu.

Waziri Jafo amesema kuwa  ili kukabilina na hali hiyo serikali imeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kukabiliana na athari hizo za kimazingira ikiwepo kuzindua kampeni ya upandaji miti pamoja na ile soma na mti katika shule za msingi na sekondari nchini.

“Nitoe shukrani kwa Rais wetu kuwa mfano na kuhamasisha utunzaji wa mazingira tangu akiwa Makamu wa Rais lakini pia Ilani ya uchaguzi ya CCM YA mwaka 2020, inaelekeza kila halmashari nchini kupanda miti milioni 1.5 kila mwaka”amesema Dkt.Jafo

Aidha Dkt. Jafo ameagiza  vibali vya ujenzi vinavyotelewa katika halmashauri nchini kuelekeza wamiliki wa maeneo kupanda miti kabla ya kuanza ujenzi ili kuendelea kuunga mkono jitihada za serikali za utunzaji wa mazingira.

Hata hivyo Waziri  Jafo amewataka watanzania kuungana kwa pamoja kushiriki maadhimisho ya wiki ya mazingira Kwa kupanda miti ili kukabiliana na athari za Mabadiliko ya tabia ya nchi.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule, amesema wameshiriki katika kampeni ya upandaji miti na kupiga marufu ya matumizi ya mifuko ya plastiki kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).

”Nampongeza Rais Samia kwa kuendeleza juhudi za kutunza mazingira katika mkaoa wa Dodoma tangu akiwa makamu wa Rais mpaka sasa.”amesema RC Senyamule

Naye Mwanafunzi wa Kidato cha nne Shule ya Sekondari ya Kiwanja cha Ndege  Shadia Ramadhan Kimaro,amesema kuwa watahakikisha wanatunza miti hiyo walio ipanda ili kuhakikisha lengo la serikali la kupanda miti katika maeneo mbalimbali nchini linatimia.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt.Selemani Jafo akiwa na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule wakiongoza zoezi la kufanya usafi lililoenda sambamba na kupanda miti katika shule ya Sekondari Kiwanja cha Ndege ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya siku mazingira Duniani itakayofanyika Juni 5, mwaka huu leo Juni 1,2023 jijini Dodoma.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt.Selemani Jafo,akiwa na mwanafunzi wakipanda mti katika shule ya Sekondari Kiwanja cha Ndege ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya siku mazingira Duniani itakayofanyika Juni 5, mwaka huu hafla iliyofanyika leo Juni 1,2023 jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt.Selemani Jafo,akimtazama  Mkuu wa mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamuleakipanda mti  katika shule ya Sekondari Kiwanja cha Ndege ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya siku mazingira Duniani itakayofanyika Juni 5, mwaka huu leo Juni 1,2023 jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt.Selemani Jafo,akizungumza na wananchi pamoja na wanafunzi mara baada ya kuongoza zoezi la kufanya usafi na kupanda miti  katika shule ya Sekondari Kiwanja cha Ndege ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya siku mazingira Duniani itakayofanyika Juni 5, mwaka huu leo Juni 1,2023 jijini Dodoma.

Mkuu wa mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule,akizungumza wakati wa zoezi la kupanda miti pamoja na kufanya usafi   katika shule ya Sekondari Kiwanja cha Ndege ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya siku mazingira Duniani itakayofanyika Juni 5, mwaka huu leo Juni 1,2023 jijini Dodoma.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Kiwanja cha Ndege Daniel Mpagama,akizungumza wakati wa zoezi la kupanda miti pamoja na kufanya usafi   katika shule hiyo  ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya siku mazingira Duniani itakayofanyika Juni 5, mwaka huu leo Juni 1,2023 jijini Dodoma.

Mwanafunzi wa Kidato cha nne Shule ya Sekondari ya Kiwanja cha Ndege  Shadia Ramadhan Kimaro,akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wenzake wakati wa zoezi la kupanda miti pamoja na kufanya usafi   katika shule hiyo ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya siku mazingira Duniani itakayofanyika Juni 5, mwaka huu leo Juni 1,2023 jijini Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt.Selemani Jafo,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya  kuongoza zoezi la kufanya usafi na kupanda miti  katika shule ya Sekondari Kiwanja cha Ndege ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya siku mazingira Duniani itakayofanyika Juni 5, mwaka huu leo Juni 1,2023 jijini Dodoma.

About the author

mzalendoeditor