Featured Kitaifa

SERIKALI KUUNDA TUME KUFUATILIA MADAWATI YA JINSIA VYUONI.

Written by mzalendoeditor

 

Naibu Waziri wa Maendeleo Ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Bi Mwanaidi Ali Khamis akifungua Mafunzo ya uanzishwaji,Uendeshaji na Ufuatiliaji wa Dawati la Jinsia Kwa Wakuu wa Vyuo na Waratibu Wa Madawati kwa Taasisi Za Elimu YaJuu Na Elimu Kati yanayofanyika Tarehe 09-10/02/2023, Mjini Morogoro.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Jinsia kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii Bi Rennie Gondwe akizungumza katika Mafunzo ya uanzishwaji,Uendeshaji na Ufuatiliaji wa Dawati la Jinsia Kwa Wakuu wa Vyuo na Waratibu Wa Madawati kwa Taasisi Za Elimu YaJuu Na Elimu Kati Yanayofanyika  Tarehe 09-10/2023 ,Mjini Morogoro.

Afisa MaedeleoyaJamii wa Mkoa wa Morogoro Tumaini Wapalila akizungumza  katika Mafunzo ya uanzishwaji,Uendeshaji na Ufuatiliaji wa Dawati la Jinsia Kwa Wakuu wa Vyuo na Waratibu Wa Madawati kwa Taasisi Za Elimu YaJuu Na Elimu Kati yanoyofanyika Tarehe 09-10/02/2023 ,Mjini Morogoro.

Kamishna Msaidizi wa Mkoa Wa Morogoro Bi Zarau Mpangule akizungumza katika Mafunzo ya uanzishwaji,Uendeshaji na Ufuatiliaji wa Dawati la Jinsia Kwa Wakuu wa Vyuo na Waratibu Wa Madawati kwa Taasisi Za Elimu YaJuu Na Elimu Kati yaliyofanyika Tarehe 09/02/2023 Mjini Morogoro.

Mwezeshaji wa Masuala ya Madawati ya Jinsia Kutoka Ofisi ya Rais -Utumishi Ndugu Staricko Meshack akiongoza Mada katika Mafunzo ya uanzishwaji,Uendeshaji na Ufuatiliaji wa Dawati la Jinsia Kwa Wakuu wa Vyuo na Waratibu Wa Madawati kwa Taasisi Za Elimu YaJuu Na Elimu Kati Yanayofanyika  Tarehe 09-10/02/2023 Mjini Morogoro.

Baadhi ya Washiriki katika Mafunzo ya uanzishwaji,Uendeshaji na Ufuatiliaji wa Dawati la Jinsia Kwa Wakuu wa Vyuo na Waratibu Wa Madawati kwa Taasisi Za Elimu YaJuu Na Elimu Kati yaliyofanyika Tarehe 09/02/2023 Mjini Morogoro.

Picha zote na kitengo cha Mawasiliano Serikalini WMJJWM.
…….
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum, Mwanaidi Ali Khamis amesema Serikali imedhamilia kuondoa Ukatili wa Kijinsia Nchini Kwa  kuja na Mpango kazi unaotekelezeka  ikiwemo Uanzishaji wa Madawati ya Kijinsia Kwenye Vyuo Vikuu na Vyuo vya kati.
Amesema hayo alipokua akifungua  Mafunzo ya uanzishwaji, Uendeshaji na Ufuatiliaji wa Dawati la Jinsia Kwa Wakuu wa Vyuo na Waratibu Wa Madawati kwa Taasisi Za Elimu ya Juu  na Elimu  kati Mafunzo yatayofanyika kwa Siku mbili mkoani Morogoro kuanzia Februari 09, 2023
“Nawapongeza Wale wote ambao wameshafungua Madawati lakini pia Nawapongeza wale ambao hawajafungua bado na wamefika hapa leo ili kujifunza namna ya kufungua na Kuendesha Madawati hayo ili kukabiliana na Ukatili unaondelea Nchini” Alisema Mwanaidi Ali Khamis.
Naibu Waziri Mwanaidi amesema uanzishwaji wa Madawati ya Jinsia  Kwenye Vyuo Vikuu na  Vyuo Vya Kati ni sehemu  ya utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Wanawake  ya Mwaka 2000 ambayo ilianza kutekelezwa Mwaka 2005.
“Tunazindua Madawati haya na Tutaunda Tume itakayofatilia Utendaji kazi wa Madawati haya kwa sababu Vitendo vya ukatili wa Kijinsia viko juu na Watoto wa kike wamekuwa Wahanga wakubwa”
Kwa upande wake Mkurugenzi msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Jinsia, Rennie Gondwe, amesema Mafunzo hayo kwa wakuu wa Vyuo Vikuu na Vyuo vya kati ni Muendelezo wa Jitihada za Serikali kupambana na Ukatili wa kijinsia
“Hii ni awamu  ya pili,Tulianza Mafunzo haya kwa Wakuu wa Vyuo vilivyopo Mkoa wa Dar es salaam, na katika awamu hii Mafunzo yanafanyika kwa Wakuu wa Vyuo  vilivyopo Pwani,Tanga na Morogoro .Tutaendelea kufanya Mafunzo haya na kuhakikisha Mikoa yote inafikiwa” amesema Gondwe.
Naye, Profesa  Musa Assad kutoka Chuo Kikuu cha Kiislamu Morogoro(Morogoro Muslim University) amesema Vitendo vya ukatili uliokithiri hasa kwenye vyuo  vinasababishwa na mmonyoko wa Maadili.
“Chanzo kikubwa cha Kuongezeka kwa Matendo haya ya Ukatili ni mmonyoko wa maadili  ulio kithiri ndani ya Jamii ,Watu hawana hofu ya Mungu   na Vijana hawana nidhamu hivyo ili kurekebisha hili inabidi tupambane kurudisha nidhamu kwa Wanajamii”alisema Profesa Assad.

About the author

mzalendoeditor