Featured Kitaifa

UTEUZI:RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI

Written by mzalendoeditor

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amempandisha cheo Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Suzan Kaganda kuwa Kamishna wa Polisi. 

Vile vile, Rais Samia amemteua Kamishna Kaganda kuwa Kamishna wa Utawala na Raslimali watu wa Jeshi la Polisi. 

Kamishna Kaganda anachukua nafasi ya Kamishna wa Polisi (CP) Benedict Wakulyamba ambaye atapangiwa kazi nyingine. 

Uteuzi huu unaanza mara moja.

Zuhura Yunus

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

About the author

mzalendoeditor